Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, vifaa kwa ajili ya ICU. Pamoja na mazingira magumu kijiografia kwenye visiwa vya Ukerewe bado Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe haikuwa na ICU. Hivi sasa tumepata mfadhili anayetujengea jengo la upasuaji (theatre). Hivyo basi, lililokuwa jengo la upasuaji linabadilishwa kuwa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) lakini patakuwa hakuna vifaa kwa ajili ya chumba hicho. Naomba Wizara isaidie kutoa vifaa kwa ajili ya chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe (Nansio).

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la umeme. Shughuli za utoaji huduma za afya zinaathiriwa sana na tatizo la umeme. Mpango wa wilaya ilikuwa kutumia shilingi milioni 70 kutoka mfumo wa RBF lakini pesa hizo zimezuiliwa mpaka sasa kutokana na mgongano kati ya Wizara mbili, pesa hizi ilikuwa zitumike kununua generator/solar system kama standby power system. Naomba Wizara itusaidie kupata ruhusa ya kutumia pesa hizi kutatua tatizo la umeme kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, gari la wagonjwa. Baada ya ajali ya MV Nyerere tarehe 20/09/2018 katika Kisiwa cha Ukara, Mheshimiwa Rais alielekeza ujenzi/ukarabati wa Kituo cha Afya Bwisya ambacho kiko hatua za mwisho kukamilika. Tarehe 15/11/2018 Mheshimiwa Waziri wa Afya wakati akijibu swali langu Bungeni aliahidi kutupatia gari la wagonjwa kwa ajili ya Kituo cha Afya Bwisya. Gari hili ni muhimu sana kuokoa maisha ya watu wetu katika visiwa hivi. Naomba gari hili litolewe na kupelekwa kwenye Kituo cha Afya Bwisya.

Mheshimiwa Naibu Spika, vituo vya afya. Ili kufika katika Kisiwa cha Irugwa inakubidi utumie zaidi ya saa nne kwa usafiri wa majini. Hali hii ya kijiografia inaweka hatarini maisha ya wananchi walio katika Visiwa hivi vya Irugwa vyenye wakazi zaidi ya 20,000. Hivyo, Kituo cha Afya kinahitajika kwenye kisiwa hiki ili kuokoa maisha ya watu wetu. Kwa kuwa wananchi wameanza ujenzi wa Kituo cha Afya Irugwa basi Wizara ituunge mkono ili tukamilishe kituo hiki kwa kukiingiza kwenye mpango wa uboreshaji wa vituo vya afya nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, watumishi na vifaa. Kwa kuwa Kituo cha Afya Bwisya kinakamilika kama ilivyo Kituo cha Afya cha Muriti, Wizara ifanye maandalizi ya kupeleka vifaa na watumishi kwenye vituo hivi bila kusahau Hospitali ya wilaya ili wananchi wetu wapate huduma ili kukidhi malengo tarajiwa.