Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia 100 kwa sababu Mheshimiwa Waziri Ummy Ally Mwalimu na Naibu Waziri, Dkt. Faustine Ndugulile wametufanyia mambo makubwa ikiwa ni pamoja na yafuatayo:-

(i) Wamehamasisha upatikanaji wa shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Namtumbo na ujenzi umekamilika.

(ii) Wamehamasisha upatikanaji wa shilingi milioni 1,500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo na ujenzi unaendelea.

(iii) Wamenihamasisha mimi Mbunge wa Namtumbo kutumia Mfuko wa Jimbo pamoja na mchango wangu binafsi kukamilisha ujenzi wa zahanati saba za Njoomlole, Mwangaza, Namanguli, Mageuzi, Ruvuma, Kitanda na Songambele, pamoja na zahanati zinazoendelea kujengwa kwa nguvu za wananchi na mchango kidogo wa mimi Mbunge za Nahimbo, Ulamboni, Mwinuko, Ukiwayuyu, Msufini, Mhangazi na Luhangano. Hatua hii ikikamilika tutakuwa tumeongeza vijiji 15 vitakavyokuwa na zahanati.

(iv) Wamehamasisha nguvu za wananchi zitumike kuunga mkono Mbunge wao katika kujenga Kituo cha Afya cha Mchomoro na kukamilisha ujenzi wa baadhi ya majengo ya Kituo cha Afya cha Lusewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna alivyotuchekecha sisi Wabunge na kugundua kipaji kikubwa cha uongozi na unyenyekevu alionao Waziri na kumteua kuwa Waziri mwenye dhamana ya afya ya Watanzania. Nampongeza sana Mheshimiwa Rais na Waziri hongera kwa kazi iliyotukuka unayoifanya. Naamini chini ya ushawishi wa Waziri akiungwa mkono na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, wana Namtumbo wanatarajia yafuatayo:-

(i) Vituo vya afya kwa umuhimu na au mpangilio huu wa Lusewa, Mchomoro, Mkongo Gulioni na Mtakanini vitaimarishwa kwa kujenga majengo mapya.

(ii) Vituo vya afya nane vilivyopo na vitakavyojengwa katika Wilaya ya Namtumbo viimarishwe kwa kupatiwa wahudumu wa afya, vifaa tiba, vitendanishi na madawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Namtumbo ina changamoto kubwa za upatikanaji wa huduma za upasuaji. Kutokana na umbali uliopo kwenda Kituo cha Afya cha Lusewa na Hospitali ya Mkoa kunakopatikana huduma hiyo ya upasuaji, naomba tusaidie kwa uharaka utakaowezekana tupatiwe fedha za kujenga Kituo hicho cha Lusewa pamoja na vituo vingine vitatu vya Mchomoro (ambako Mheshimiwa Rais ameahidi kuchangia shilingi milioni 100), Mkongo Gulioni (kinahudumia Kata sita za Mkongo Gulioni, Mkongo, Luchili, Limamu, Ligera na Lisimonji na mwisho Kituo cha Mtakanini kilichoahidiwa na Mheshimiwa Benjamini William Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli huduma za afya bure kwa watoto wa chini ya miaka mitano, wajawazito na wazee wenye umri zaidi ya miaka 60 ni changamoto kubwa lakini kabla ya miundombinu ya afya kukamilika kujengwa ni kazi bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, nirudie kukupongeza na kukushukuru kwa namna unavyoakisi dhamira ya Mheshimiwa Rais ya kuwagusa na kuwainua wanyonge katika sekta zako hususan sekta ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.