Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Waziri na Naibu Waziri pamoja na timu nzima kwa kazi nzuri ya bajeti waliyotuletea.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeahidiwa gari la wagonjwa Kituo cha Afya Engusero. Tunaomba yatakapopatikana basi tupatiwe gari.

Mheshimiwa Naibu Spika, upungufu wa watumishi. Tuna watumishi 296 na upungufu ni watumishi 210, tunaomba tupatiwe watumishi hao kwa ajili ya zahanati, vituo vya afya na hospitali ya wilaya. Vilevile, tunaomba Waziri kutembelea Wilaya ya Kiteto kuzungumza na watumishi na kuangalia uchakavu wa Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho naunga mkono hoja, Mungu awabariki.