Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja sambamba na kupompongeza Mheshimiwa Waziri kwa wasilisho lake zuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuzuia miili ya marehemu (maiti) kama sababu ya deni la matibabu hususani katika Hospitali za Muhimbili na Mloganzila ni kero kubwa sana na ni jambo ambalo limekuwa likiigombanisha Serikali yetu na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali iliangalie suala hili na ilifanyie uamuzi wa kulifuta haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni mapambano dhidi ya malaria. Tuna kiwanda chetu pale Kibaha cha kutengeneza dawa ya kuulia vimelea vya vidudu vya malaria. Kiwanda kile kinakabiliwa na changamoto ya soko. Lile agizo la Mheshimiwa Rais kuwa kila Halmashauri ikanunue dawa pale halijatekelezwa sawasawa. Niiombe Serikali yangu sikivu kukiokoa kiwanda kile kwa kukipatia soko la uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru na naunga mkono hoja.