Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto wa kike, hasa majumbani na wapatapo shida hawana pa kuwatunzia wakati usuluhisho unaendelea hivyo kupelekea kurudi katika majumba yao ambayo sio salama kwa wakati huo. Nashauri Serikali ijenge majengo salama kwa usalama wa waathirika.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na upungufu wa wodi za wanawake, hasa katika Hospitali ya Makandana, Tukuyu. Tunaomba Wizara kwa kusaidiana na Halmashauri ya Rungwe kutatua tatizo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimba za utotoni. Tunaomba Wizara itoe tamko kwa mabinti wapatao mimba katika umri mdogo kurudi shule hasa walio chini ya miaka 15 kwani kutorudi shuleni kunapoteza haki yao ya kupata elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, dawa/chanjo ya mbwa. Kwa wagonjwa waliong’atwa na mbwa matibabu ni ghali sana. Tunaomba Wizara ipunguze kama sio kutoa bure chanjo hizo kwa waathirika.

Mheshimiwa Naibu Spika, vipodozi hatarishi. Wizara na wadau wa afya kwa pamoja wafuatilie madawa/vipodozi hatarishi vinavyoathiri afya za wanawake na watoto. Kumekuwa na madawa yasiyo rasmi katika maduka mengi na dawa kama za kuongeza makalio, matiti, uume na hata wanaojichubua, Wizara ya Afya, TFDA na TBS kwa umoja wasaidie jamii yetu kutopata matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, uhaba wa watumishi. Wizara ipeleke wataalam hasa wa magonjwa ya wanawake na watoto katika Mkoa wa Mbeya, Wilaya za Chunya na Mbarali, ndiyo zenye changamoto kubwa.