Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kuhusu wahudumu wa afya katika ngazi ya jamii. Serikali imetoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii 10,000. Wahudumu hawa wamekuwa msaada mkubwa sana kwenye ngazi ya jamii kwa kuzuia vifo vya watoto na akina mama lakini Serikali haiajiri tena wahudumu hawa. Naomba Serikali ione namna ya kuwapatia motisha na siyo mishahara.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, bima ya afya. Naomba Serikali iharakishe Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kuwa matibabu ni gharama na watu wengi wanapoteza maisha kwa kukosa pesa za matibabu. Pia watu wanaotumia bima wanakosa baadhi ya dawa za magonjwa makubwa kama moyo na mengine. Hivyo, naomba bima hizo ziingize matibabu yote na siyo baadhi ya magonjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatu, Maafisa Ustawi wa Jamii. Maafisa hawa ni muhimu sana lakini hawana bajeti ya kutosha. Mara nyingi wanatumia fedha zao za mfukoni kwa ajili ya kazi za kutembelea na kufuatilia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi. Hivyo, naomba Maafisa Ustawi wa Jamii wapewe bajeti ya kutosha kwa ajili ya kutembelea na kufuatilia familia mbalimbali zenye matatizo pamoja na watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nne, ada ya usajili wa dental clinics. Gharama za usajili wa clinic hizi ya Sh.1,000,000 ni kubwa. Naomba gharama hizo zipunguzwe kwani ni huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.