Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa mimi kupata fursa ya kuzungumza kidogo kwa ajili ya kuchangia hotuba ya bajeti hii ya Wizara ya Afya. Nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuisimamia Wizara hii, lakini kusimamia na kupigania afya za Watanzania. Tunao ushahidi, tunaona kwa macho, Hospitali zinajengwa, hospitali za rufaa na vinajegwa vituo vya afya kila kona. Kwa kweli, kazi kubwa inafanyika, lakini nimpongeze sana mama yetu mama Ummy, Watanzania wanamwona namna anavyofanya kazi na hakika Mwenyezi Mungu atamlipa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikumbushe mambo machache yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, Mheshimiwa Ummy alikuja Mtwara wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais katika Mkoa wa Mtwara, Mheshimiwa Ummy alisikia kilio cha Wabunge wa Mtwara na Wabunge wa Kusini kwa ujumla pamoja na wananchi kuhusiana na suala zima la Hospitali ya Kanda ya Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ummy kwa kweli moyo wake mwema, uendelee hivyo hivyo kwa kuhakikisha kwamba hospitali hii inajengwa na inakamilika kwa sababu kwa muda mrefu ujenzi ule umesimama na sisi tunaisubiri kwa hamu sana hospitali hiyo ili tuweze kupata huduma za afya kubwa kubwa kama wanavyopata katika maeneo mengine waliopata Hospitali za Kanda za Rufaa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nitumie fursa hii kumkumbusha Mheshimiwa Ummy alipokuja Masasi katika ziara yake ya kikazi, alipata fursa ya kufanya mkutano wa hadhara. Katika mkutano ule tulimwomba ambulance moja na aliahidi kutupatia, tunaomba moyo wake mwema, uendelee hivyo hivyo atusaidie tuweze kupata ambulance hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakumbusha tena Mheshimiwa Ummy kwamba alipata fursa ya kutembelea Hospitali ya Mkomaindo, aliona changamoto kubwa tuliyonayo kwenye upande wa x-ray, x-ray ni chakavu na haifanyi kazi. Tunamwomba moyo wake uendelee kuwaangalia kwa jicho la kipekee watu wa Masasi atuletee x-ray mpya ya ki-digital kama katika maeneo mengine ili wananchi waweze kupata huduma inayostahili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimkumbushe tena dada yetu Mheshimiwa Ummy, kwamba ameona hali halisi ya Hospitali yetu ya Mkomaindo na namna ambavyo chumba cha upasuaji hakiwezi hata kuchukua zaidi ya mgonjwa mmoja katika kutoa huduma. Tunaomba mabadiliko makubwa ya chumba hiki ili wananchi wetu waweze kupata huduma inayostahiki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimkumbushe tena Mheshimiwa Ummy, kwamba kama ilivyo katika maeneo mengine, tuna uhaba mkubwa wa Madaktari na wahudumu wa afya katika Jimbo la Masasi, tunaomba pia atuangalie kwa mikono miwili.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema maneno hayo, naunga mkono hoja. (Makofi)