Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kipaumbele cha juu kabisa, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa hii nafasi ya kufanya shughuli ya leo. Pia nawashukuru wananchi wa Biharamulo kwa kuendelea kuniunga mkono, lakini kwa namna ya pekee napenda kuipongeza Serikali, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Sekta hii ya Afya mambo yanaonekana, lakini Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile na wasaidizi wenu Katibu Mkuu na wengine wote tunawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushahidi uko wazi, mimi nitatoa ushahidi mmoja kwamba mkononi kwangu nina ripoti, utafiti uliofanywa na Taasisi ya Institute for Health Metrics and Evaluation, moja ya mambo ambayo wamepima ni habari ya maternal mortality kwa watoto wa chini ya miaka mitano na infants wale chini ya mwaka mmoja, inaonesha kabisa takwimu ziko wazi hapo kwamba hatujafika tunapotakiwa kufika, lakini tunakwenda vizuri kulingana na matarajio namna wanavyopima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nawapongeza sana, lakini tumesikia hapa, Mheshimiwa Mbunge mmoja amesema namna ambavyo Wizara hii inapata pesa kidogo ukilinganisha na mahitaji ambalo sio jambo zuri, lakini hata Mheshimiwa Ummy na Mheshimiwa Ndugulile na timu yao, kwa kweli wamejitahidi sana kuratibu wadau wengine wa nje ya Serikali. Ndiyo maana mambo mengine yanakwenda, ukipata fursa ya kuwa nao karibu utaona hilo na kweli huwa linanitia moyo sana, naona mwanga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niseme mawili ya Biharamulo; moja tunashukuru tumejengewa Kituo cha Afya Nemba, lakini kinaleta mahitaji kwa sasa tutafanya upasuaji pale wa akinamama wajawazito, wale wanaohitaji upasuaji, tunahitaji ambulance, jiografia ya Biharamulo ni ngumu sana kwa sasa tuna Kituo Nyakahura na Nyakanazi ambavyo ni mbali sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambasamba na hilo, tunahitaji wataalam wengine wa dawa za usingizi, yako matukio kadhaa ya upungufu yanayosababisha vifo vya akinamama kutokana na upungufu wa wale wataalam wa dawa za usingizi. Tuna Madaktari, ama MD mmoja ama wawili, wako kwenye hivyo vituo, lakini kwa sababu watu wa usingizi hawatoshi, mara nyingine ucheleweshwaji inakuwa haiwezekani kufanya upasuaji kwenye Kituo cha Afya na safari ya kwenda Biharamulo Mjini kwa ajili ya upasuaji inakuwa ndefu inasababisha vifo. Hayo ndiyo mahitaji yetu mawili makubwa kwa Biharamulo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nije suala la Kitaifa, pamoja na pongezi na kazi nzuri inayofanyika yako maeneo ya kuboresha. Ukitazama ripoti hii hii ya Institute of Health Metrics and Evaluation, inasema kwa mwaka 2017 wamelinganisha 2007 na 2017, hii ni taasisi maarufu sana duniani na inaheshimika, wame-rank wameweka uwiano, wamepanga ule uzito wa sababu za vifo kwenye nchi yetu hii. Katika sababu hizo, ziko ambazo zinatokana na UKIMWI, TB, Malaria lakini hata na magonjwa ya kuhara ni miongoni mwa sababu kumi za vifo ambavyo zinachukua uzito wa juu. Metrics

Mheshimiwa Naibu Spika, na sababu za vifo, kabla ya wakati, yaani zile pre-mature death wame-rank mambo hapo, kuna tuberculosis, lakini kuna protein energy malnutrition, mambo ya utapiamlo, mambo yanayozuilika kabisa na sababu za ulemavu, inayoongoza kabisa ni dietary iron deficiency na ukiangalia zaidi kwenye ripoti yao wanasema, vifo pamoja na ulemavu kwa pamoja sababu inayoongoza ni malnutrition, utapiamlo, yaani nchi hii tuna tatizo kubwa la utapiamlo, pamoja na kufanya kazi vizuri sana huko kwenye tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ningependa, nijikite zaidi kwenye utapiamlo huo, Sera ya lishe nchi hii, imepitwa na wakati, toka mwaka 1992. Kwa bahati mbaya, ilikuwa inatazama zaidi mchango wa lishe kutoka kwenye Sekta ya Afya, haitazami mchango wa lishe kutoka kwenye sekta nyingine, hili ni tatizo. Tunaomba tufanye mapitio ya Sera, kama asilimia, tatizo linaloongoza kwa habari ya vifo na ulemavu kwa pamoja, namba moja ni utapiamlo wala sio kipindupindu, sio jambo lingine wala sio malaria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima twende kwenye Sera yetu, tuone namna gani sekta zote zitaingia. Nakumbuka mwaka jana, waliwaita Wakuu wa Mikoa hapa, nikaona wanaweka sahihi, lilikuwa ni jambo zuri, lakini nikawa najiuliza hivi hizi sahihi zitatusaidia, kama hatuna framework? Pia sijasikia ushahidi wowote kwamba hizo sahihi zimesaidia, wameleta improvement, ni kwa sababu lazima likae kimfumo, tuzialike Sera zote kisera na tunaomba katika hili, ikae Sera ya Lishe sio kuchukua habari ya lishe kuiweka kwenye Sera ya Afya, kwa sababu hili jambo ni mtambuka na kubwa. Naomba kusema kwamba hili tutalipigia kelele sana. Tunaomba Sera ya Lishe ije haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, usafi; moja ya sababu zinazosababisha vifo, ukichanganya vifo na ulemavu kwa pamoja, ni habari ya wash, mtu anatoka kujisaidia hanawi mikono, anakuja kumsalimia mwenzake na hapa ukiangalia kama mtu angekuwa anapima watu tunavyosalimiana, hapa kwa mikono lakini asilimia zaidi ya sabini ngapi hawanawi mikono baada ya kujisaidia. Hili linahitaji elimu tu na wamesema Wabunge wengi hapa, twende kule kwenye zahanati na vituo vya afya tuweke wahudumu wa afya wa kwenda kuelimisha vijijini wa kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeona kwenye Ikama ya Watumishi wa Afya wanayo ya zahanati inasema Clinical Officer kwa siku aone wagonjwa 40. Mtu wa madawa kwa siku ahudumie prescription 40, lakini ikifika kwa yule Community Health Worker inasema aunganishe tu kituo na kijijini, haimpi kwamba leo katazame vyoo saba ukatazame wangapi wameweka sehemu za kunawa, twende huko, tuondoke kwenye tiba sasa tumeshafanya vizuri, twende kwenye afya. Watanzania wanahitaji Afya, nimesikia watu wanawapongeza Madaktari na mimi nawapongeza, lakini ifikie hatua, tuanze kupongeza, tunawapongeza Mabwana Afya, wamehamasisha sasa huku hatuharishi, kwa sababu ukiangalia hapa inasema asilimia 2.7 ya wananchi nchi hii hawana vyoo kabisa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)