Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Nami niendelee kuungana na Waheshimiwa Wabunge wa Chama cha Mapinduzi katika kuhakikisha kwamba tunaendelea kumpongeza Mheshimiwa Waziri Ummy na Naibu wake na timu nzima ya Wizara hii ya Afya katika kuhakikisha kwamba wanaendelea kuchapa kazi na kazi zao zinaonekana. Mheshimiwa mmoja amesema aliye na macho haambiwi tazama, kwa sababu kazi hizi zinaonekana, tunaendelea kuboresha afya za Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia niendelee kumpongeza na kumshukuru Mheshimiwa Ummy Mwalimu kwa kufanya ziara katika Mkoa wetu wa Lindi. Imeleta tija sana na faida kubwa kwetu, lakini ameweza kujionea changamoto mbalimbali ambazo zipo katika Mkoa wetu wa Lindi katika eneo hili la vituo vya afya ambavyo vinaendelea kujengwa. Vipo ambavyo vimekamilika na vipo ambavyo havijakamilika lakini vinaendelea viko katika hatua nzuri sana, tunaendelea kuvisimamia kuhakikisha kwamba vituo hivi vinakamilika na vianze mara moja kutoa huduma. Vile vile vipo vituo vya afya ambavyo vimekamilika; Kituo cha Mnazi Mmoja pale Lindi Manispaa, lakini kituo kimoja pale Lindi Vijijini, kule Nyangamala, tunasubiri tu ufunguzi ufanyike vituo hivi vianze kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunamshukuru Mheshimiwa Ummy Mwalimu, alifanya uzinduzi wa upimaji wa Saratani ya Shingo ya Kizazi pale Sokoine, Lindi Manispaa, huduma hii imeweza kusaidia kuwafikia wanawake wengi wameweza kujitokeza katika kuhakikisha kwamba wamekwenda kupima tatizo hili la Saratani ya Shingo ya Kizazi. Niendelee kuipongeza Serikali na niishauri Serikali kuendelea kutoa huduma hii ya mobile katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania kuhakikisha kwamba wanawake wengi wanajitokeza kuendelea kupima tatizo hili ambalo linaonekana sasa linakua kwa kasi kubwa katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kufanya kampeni ya utoaji wa chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa watoto wetu wa kike kuanzia umri wa miaka 14 japokuwa tunapata changamoto ya kwamba wazazi wa watoto hawa hawawaruhusu kupata hii chanjo. Naomba tuendelee kutoa elimu kwa wazazi hawa na watoto wetu ili waweze kupata kinga hii ambayo inatolewa na Serikali kwa sababu tatizo hili mbele ya safari linasababisha wanawake kunyanyapaliwa na waume zao kutokana na tatizo hili la kansa ya shingo ya kizazi na wanawake wengi wanapoteza maisha kutokana na tatizo hili kubwa ambalo linaendelea kukua katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulishirikiana na Mheshimiwa Ummy Mwalimu katika kuhakikisha kwamba tunahamasisha wananchi kujiunga na NHIF katika Mkoa wetu wa Lindi. Tatizo lililopo ni kwamba wananchi wengi hawana elimu ya kutosha ya upatikanaji wa kadi hizi za bima ya afya. Nashuhudia pale Ruangwa alitoa elimu na wananchi palepale hospitali walidiriki kukata na kujiunga na NHIF. Kwa hiyo, suala kubwa ni tuendelee na kampeni kuwahamasisha wananchi wetu kujiunga na NHIF ili waweze kupata huduma ya matibabu pale wanapopatwa na matatizo na inasaidia pale wanapokuwa hawana fedha, basi kupata matibabu bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, la msingi ni kuendelea kuimarisha vituo vyetu vya afya vyote viwe na dawa za kutosha ili wananchi wale wenye bima za afya wasikate tamaa na itakuwa ni njia nzuri ya kuwafanya hao wenye bima ya afya kuendelea kuhamasisha watu wengine ili waweze kujiunga na wao katika mpango huu wa bima ya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mafanikio makubwa tuliyoyapata katika ujenzi wa vituo hivi vya afya, bado tunazo changamoto mbalimbali. Ukiangalia katika Mkoa wetu wa Lindi eneo hili la watumishi tuna changamoto kubwa sana na Mheshimiwa Waziri Ummy alipokuja alipata taarifa ya mahitaji ya watumishi katika Mkoa wa Lindi. Mahitaji yalikuwa ni watumishi 4,898 lakini watumishi waliopo ni 1,784, sawa na asilimia 36 na pungufu ilikuwa ni 3,114 sawa na asilimia 64. Kwa hiyo upungufu huu wa watumishi katika eneo hili la afya katika Mkoa wa Lindi ni kubwa sana na ni changamoto kwa sababu wananchi wengi wanakosa kupata huduma hii kwa kukosa Madaktari na watumishi mbalimbali katika maeneo haya ya vituo vyetu vya afya, zahanati na hospitali ambazo zipo. Kwa hiyo, tunamwomba Mheshimiwa Ummy Mwalimu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)