Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nfasi. Naomba nianze kabisa kuungana na Taifa kwa ujumla katika simanzi kubwa iliyotukuta kuondokewa na mojawapo ya Mtanzania maarufu aliyefanya mambo mengi, Dkt. Reginald Abrahamu Mengi. Nachukua nafasi hii kutoa pole sana kwa wanafamilia na pia kumshukuru sana kwa msaada wake alioutoa kwa watu mbalimbali, hususan kwa sisi ambao tunashughulikia elimu bora kwa wasichana ambao hawana uwezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mengi alikuwa ni mtu mkarimu na waswahili wanasema kutoa ni moyo sio utajiri. Kwa hiyo, tunaomba sana familia yake iyachukue kama yalivyokuja na Mwenyezi Mungu ampe pumziko la milele.

Mheshimiwa Naibu Spika, sina budi kusema kwamba, pigo kubwa kwa sababu, siku kadhaa zilizopita wakati Marehemu Ruge Mutahaba amefariki, pia na Ephraim Kibonde wote tulikuwa katika chumba kimoja pale Karimjee, lakini hizo ndizo njia za Mwenyezi Mungu ni pigo kubwa kwa Taifa. Na ninasimama hapa kwa majonzi makubwa leo, jana tumempoteza Prof. Robert Mabele wa Chuo Kikuu cha Dar- es-Salaam na yeye nichukue nafasi hii kumshukuru kwa mchango wake katika kufundisha wachumi wengi ndani ya chumba hiki, nadhani na Waziri wetu wa Fedha ni wanafunzi wake kwa hiyo, ni pigo kubwa kwa Taifa, Mwenyezi Mungu amrehemu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana sasa niende kwenye ajenda, nianze kuungana pia na wengine kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Ummy na Makamu wake kwa kazi nzuri wanayoifanya. Mheshimiwa Dkt. Ndugulile alipata nafasi kunitembelea kule na kwa sababu yeye ni daktari mambo ya Muleba aliyaona kwa karibu na alifuata hata na Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu ulifika pale Rubya Hospital ukatembelea hospitali teule ya wilaya, kwa hiyo, naomba nianzie hapo.

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa nchi hii katika kutoa huduma ya afya ambayo sina budi kupongeza juhudi kubwa ambazo zimefanyika katika Awamu ya Tano. Juhudi ambazo tumesikia wakati Waziri Jafo anaorodhesha hospitali ambazo tumejenga za wilaya ni jambo la kujivunia. Mwemyewe kwa upande wa Muleba Kusini tunashukuru kwamba, vituo vya afya viwili Kimea na Kaigara vimeimarishwa, upasuaji sasa hivi unaendelea. Jambo hili kwa kweli, tunashukuru sana juhudi hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa Hospitali Teule ya Wilaya ya Rubya naomba niseme kwamba, nikiiangalia Rubya kwa karibu, lakini na hospitali nyingine kwa ujumla hizi zinaitwa designated hospitals. Utaratibu wa public private partnership naomba nichukue nafasi hii kusema kwamba, ni utaratibu muhimu sana. Na tunapoboresha hospitali za Serikali tusisahau pia umuhimu wa kuhakikisha kwamba, zole ambazo tulikuwanazo nazo tunalinda uwezo wake kwa sababu, isije ikawa ni wazungu wanesema, you rob Peter to pay Paul; tusimuibie Paulo kumlipa Petro, hapa inatkiwa balance.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaomba sana Mheshimiwa Waziri anapojumuisha tusikie mkakati alionao kuhakikisha kwamba, hizo hospitali tulizokuwanazo zinaendelea pia, kufaidika na hii partnership iliyokuwepo la sivyo tunaweza tukajikuta kwamba, hospitali zinadidimia. Sina budi kusema kwamba, hospitali sio majengo, hospitali ni huduma na katika hili niunganishe hapohapo kusema kwamba, Mheshimiwa Waziri pia, aangalie hali halisi ya referral hospital zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza sana juhudi za Serikali ya Awamu ya Nne iliyokamilisha Hospitali ya Mloganzila, lakini Mloganzila hospitali majengo, hakuna Hospital town pale kwa ajili ya madaktari kukaa karibu na hospitali. Na hata huyo Profesa Mabele ambaye namsema kafia Mloganzila nilikwenda kumuangalia tu juzi nikakuta kwamba, kama kuna dharura daktari anafikaje Mloganzila? Kwa hiyo, nadhani kuna haja ya kufanya uwekezaji kuhakikisha kwamba, kituo kinafanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye Hospitali ya Rubya ninaomba sana Mheshimiwa Waziri Ummy unapafahamu, ulikuwa unataka kuleta mashine ya viral load kwa ajili ya upimaji. Sasa hivi mashine hiyo tunasikia kwamba, imehamishwa imepelekwa Bukoba na vifaa vingine. Hata na watumishi wa maabara tunapozungumza hospitali haina any degree holder kwenye pharmacy.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni hospitali inayohudumia wilaya, wakazi laki saba. Kama una wananchi 700,000, huna maabara ambayo ina a qualified technician unaona kwamba, hapo huwezi kwa kweli, kutoa huduma inayostahiki. Kitengo cha meno pale kiko katika hali mbaya kwa hiyo, nafikiria kwamba, Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri mnayoifanya na utaalamu mlionao ni muhimu sana kwamba, pia, kuweko na uboreshaji tuhakikishe kwamba, hospitali zetu za zamani hazitasambaratika.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mwisho kabisa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)