Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Dakika zangu umenipatia chache lakini hizi hizi naona zinaweza kutosha kidogo kwa mambo niliyokuwa nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia kuwa na hali ya uzima na afya na kutujaalia kuwa na mfungo wa Ramadan na leo ndiyo kwanza siku ya kwanza. Kwa hiyo Mungu atusaidie tuifunge Ramadan kwa salama ana amani na tupendane sote humu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake ya Wizara ya Afya iliyojaa maono, haina mjadala. Mzungu amesema no discussion. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuendelea, dakika zangu tano nataka kuzungumzia suala la mradi wa magonjwa yasiyo ambukizika. Kuna magonjwa yasiyo ambukiziki ni magonjwa ya sukari, presha pamoja na magonjwa ya shinikizo la damu. Magonjwa ya sukari haya ni magonjwa tutasema mfano kama yanapunguza ile hofu ya mgonjwa hasa atakapokuwa anapata dawa zake za uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wagonjwa wa sukari ambao wagonjwa hawa wa sukari na presha zinaendana pamoja na shinikizo la damu lakini wagonjwa hawa wengine wanyonge, maskini hawana hata ile bima ya kuweza kununulia zile dawa zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, dawa ziko nyingi sana nakupongeza sana lakini hizi dawa kama huna pesa au huma bima unakuwa huwezi kuzinunua baadhi ya dawa nyingine maana kuna dawa nyingine zinashusha hata sukari, unapata nne, tano, saba, nane lakini kuna dawa nyingine zinakuwa hazishushi. Sukari ile inakuwa inapanda pamoja na presha hasa kuna dawa hizi za mizizi ambazo tunapewa humu nje. Dawa zile Mheshimiwa Waziri yanaua kongosho la eucilin kwa hiyo, yanapoua lile kongosho la eucilin basi uhakikishe wewe mgonjwa wa sukari tayari umeshapata ganzi, tayari umeshapata hofu, tayari unakuwa huna nguvu za mwili ambao ukaweza kufanya harakati zako ulizokuwa nazo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, nakuomba naiomba Serikali yangu hivi sasa hivi kwamba itafute dawa ambazo zipunguze gharama ili na wale wengine waliokuwa hawana zile bima au hawana ile pesa waweze kuzinunua hizi dawa.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Mwantumu Dau.

MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ilikuwa suala langu hili la kuhusu magonjwa yasiyoambukizi ni hili. lakini la pili, nataka kuzungumzia…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwantumu muda wako umekwisha nashukuru sana kwa mchango mzuri. (Makofi)

MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja lakini mmenipa dakika kidogo. Ahsante sana, pia nashukuru. (Makofi)