Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumshukuru Mungu kunipa uzima kuwepo mahali hapa jioni ya leo niweze kuchangia Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ripoti ya CAG ya 2017/18 inaonesha kuna ujenzi wa hospitali m bili za rufaa Mkoa huu mmoja na hospitali hizo zinazojengwa Chato imetengewa bilioni 9.9, Geita billioni 5.9 kwa mkoa mmoja tu ni bilioni 16. Hizo ni hospitali za rufaa kwenye mkoa mmoja. Ukizingatia huu mkoa wa Geita, wananchi wa mkoa huo wapo milioni 1.7. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuchukue Kanda ya Kusini yenye mikoa mitatu, Lindi, Mtwara, Ruvuma haina hata hospitali ya rufaa na tukichukua hii mikoa mitatu ina watu milioni 3.6. Ninashindwa kuelewa Wizara ina maana gani? Tunaposema tunataka kujenga hospitali za rufaa tunaangalia uwiano upi kwa wananchi wa maeneo husika? Nitamtaka Waziri anapokuja kuhitimisha hoja hii aje na majibu yanayotuambia mpango wa Wizara yake inaangalia eneo labda la kiongozi fulani lakini sio inaangalia tija kwa wananchi waliopo eneo husika kupeleka hospitali za rufaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninafikiri tunazungumzia upungufu wa watumishi Sekta ya Afya tena hawa watumishi wenye ujuzi wa kutoa huduma kwenye vituo. Tunapozungumzia hivi sasa hivi tuna upungufu wa asilimia 56, ni tatizo kubwa sana kwa Taifa. Nafikiri kwenye kitabu cha maendeleo sijaona mahali ambapo pameonesha kwamba katika mikoa ile niliyoitaja mitatu ya Kusini kwenye kitavbu cha maendeleo hakijatengewa hata bajeti. Hivi watu wa Kusini sisi tuna tatizo gani? Geita ni mkoa mpya kama Mkoa wa Njombe, Njombe ni ukweli usiopingika kuna matatizo yaliyozidi kuliko hata watu wa Geita lakini hakuna kinachoonekana kama Serikali inaangaliaje hivi vipaumbele katika hii mikoa mipya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nije na uwiano. Kwenye kitabu hiki nimejaribu kusoma vizuri sana, sikuona mahali panapoonyesha hospitali teule ya Kibong’oto iliyopo Mkoani Kilimanjaro kama imetengewa fedha ili waweze kuiboresha ukiangaliano uwiano wa ugonjwa huu wa kifua kikuu kuwa watu 10 wazima, watu 30 wanaohakikiwa wanakuwa na kifua kikuu. Ukiangalia kwenye uwiano wa Watanzania milioni 55 kwa sasa ukipiga mahesabu ina maana Taifa letu lina watu wenye ugonjwa wa Kifua kifuu milioni18, hili si jambo dogo! Milioni 18 ambapo ukiangalia asilimia 30 ya wenye…

T A A R I F A

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najua yeye ndiye mwenye Wizara yake tunayoijadili, bado alikuwa na muda mkubwa wa kuja kujibu hii hoja kama nilivyomtaka wakati wa kujibu aje aseme.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Suzan, kama unakosea haifai kwa sababu unakuwa unapotosha Umma na yeye ndiyo anaelewa…

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea. Niachie niendelee. Nimesema katika watu 10,000 wazima, wapato 30 ambao wana hakikiwa, wana ugonjwa wa TB, tumefundishwa, NGO zinakuja hapa kutoa elimu na watu tunaandika ili tuje tuisaidie Serikali katika kuboresha kwenye bajeti. Sio kosa langu mimi, basi ni kosa la NGO zinazokuja kuelimisha kama wanatupotosha sio hoja yangu mimi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee. Basi sasa katika hilo kama alivyosema Waziri hata kwa idadi hiyo, hiyo hospitali niliyoitaja kwneye kitabu chako hiki hujaitengea bajeti ili uiboreshe vizuri. Naomba niendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba unilinde, umenipa muda mdogo nilikuwa na dakika 10 sasa dakika zangu nimepewa chache. Huduma ya lishe, nchi yetu ya Tanzania duniani ni ya 10, Afrika ni ya tatu, nchi ya Tanzania ilivyo, Mungu alivyoipendelea ina eneo kubwa, tunazalisha aina ya vyakula tatizo hapa ni elimu na elimu tunaipata wapi? Kwa Maafisa Maendeleo wa Jamii ambao katika Taifa letu wamekuwa ni wachache sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa maafisa maendeleo wa jamii wanaishia ngazi ya kati, elimu hii ili itusaidie kuangalia watu wapate chakula, lishe bora ianzie kwenye vitongoji vyetu tunakoishi. Tuitake Serikali ianjiri maana vyuo vya maendeleo ya jamii vimepata wahitimu wengi ambao hawa na ajira, wamebaki mitaani. Hawa wangetoa elimu ya lishe nafikiri Taifa letu lisingefikia mahali hapa kulinganisha na neema ambazo Mungu nchi ya Tanzania aliipa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naingia kwenye suala la tiba asilia. Tulikuwa na mafunzo Mkoa wetu wa Iringa mwezi uliopita ambapo kuna NGO iliendesha hayo mafunzo. Mkoa wa Iringa tu hili naomba Waziri ulichukulie kwa sababu waliomba Wizara iangalie upya jinsi ya kusajili waganga wa jadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Iringa tu hadi sasa tunapozungumza umeshasajili waganga 878 na ambao hawajasajiliwa ni 900. Kwanini watu wameomba tulilete Bungeni? Imeonekana katika usajili huu nafikiri hakuna mpango mkakati ambao umeelekezwa hawa wanasajiliwa na afisa watendaji kwenye kata kiasi kwamba mtu anatoa hela anasajiliwa wanaanza kupotosha imani za watu ambao wanawadanganya kuwa akienda anasema kaleta kiungo cha albino…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa na muda umekwisha.

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani

MWENYEKITI: Ahsante sana kwa kuunga mkono hoja.

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Nimesema naunga mkono hoja hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dau tuendelee.

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Siwezi kuunga hoja ya Dada Ummy.