Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi, kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa uzima na kuweza kufanya mambo ya kuwasaidia Watanzania katika kujiletea maendeleo. Awali ya yote nitoe pole nyingi kwa msiba wa Dkt. Reginald Mengi, ni kweli kwamba maandiko yanasema hakuna mji udumuo na kwamba kila nafsi itaonja mauti. Basi naomba kifo cha Dkt. Mengi kiwe ni fundisho kwa sisi tulio baki kwam ba iko siku yetu na kila mmoja ataulizwa nini amefanya kwa ajili ya jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kumpongeza sana Waziri wa Afya pamoja na Naibu wake, Katibu Mkuu na viongozi wote kwa namna wanavyoiongoza Wizara hii. Wilaya ya Wanging’ombe haina hospitali ya wilaya, nishukuru katiak bajeti ya mwaka huu fedha zimetolewa, tumeanza kujenga hospitali ya Wilaya na nafikiri kufika mwezi wa Saba tutakuwa tumemaliza. Lakini pia nishukuru kwa uboreshaji wa vituo vya afya viwili, kituo cha Wa nging’ombe pamoja na Parangawani. Wananchi wale walikuwa wameanza kujenga kwa nguvu zao na Serikali imewaunga mkono. Basi naomba kwa sababu wameshamaliza, vifaa tiba na vifaa vinavyohitajika pamoja na wahudumu wa hospitali zile waweze kuleta m apema ili huduma ya afya iweze kufanyika.

Mheshimwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka 2018/19 na kwa sababu Serikali ni moja, na nimemuona Mheshimiwa Dkt. Mpango yuko hapa, kulikuwa na ahadi ya kutolewa karibu billioni moja kwa kila halmashauri ili kukamilisha maboma ya vituo vya afya pamoja na shule za msingi. Fedha ile haikutolewa mpaka leo na sisi tulikuwa tumewahamasisha wananchi wamejenga maboma kwa wingi kweli kweli. Wilaya ya Wanging’ombe tunavyo vituo vya afya saba, zahanati 13, wodi za wazazi mbili, nyumba za waganga tatu ambazo kukamilisha kwao kunahitaji karibu bilioni 2.5.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wananchi wale walikuwa wanategemea sana fedha ile itoke. Naomba sana kabla ya Bunge hili sisi ili tusionekane tunawadanganya wananchi. Tujitahidi Serikali iweze kuleta fedha hizi ili kwa juhudi hizi ambazo wananchi wanaendelea kuunga mkono kazi nzuri anayofanya Dkt. John Pombe Magufuli, basi fedha zile zitoke tuweze kukamilisha majengo haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Awamu ya Nne, Rais Dkt. Kikwete aliahidi gari la wagonjwa katika kituo cha afya cha Makoga. Sasa ni miaka sita gari lile halijapatikana. Najua Serikali yangu ni sikivu, basi naomba sana gari la wagonjwa lililoahidiwa na Rais liweze kutolewa kwa kituo cha afya cha Makoga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie pia katika hoja ya Waziri, kwanza pia nimpongeze nimeona pamoja na kwamba yeye ni Waziri wa Afya, amekuwa anashiriki katika ujenzi wa bweni la watoto wa kike katika sekondari ya Kilale katika Jiji la Tanga. Basi nimtakie kila la kheri hiyo azma aliyonayo katika wananchi wa Tanga. Lakini nikukaribishe pia kule Wilaya ya Wanging’ombe tuna shule ya wasichana ya Maria Nyerere na tuna tatizo la bwalo, basi naomba pia ukiweza kuja kuhamasisha wananchi tutafurahi sana ukitembelea wilaya ile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia Bima ya Afya kwa wote, ni kweli katika eneo hili nafikiri tufanye kazi ya ziada zaidi. Hizi bima za afya ambazo zinatolewa katika kiwango cha kaya inakuwa haikidhi kupata matibabu wakienda kwenye hospitali zingine. Sasa nilifikiri huu mpango wa kuleta hii sheria tuwe na Bima ya Afya kwa wote. Kwa kweli naiunga mkono na ningeomba jambo hili lifanywe haraka. Lisichukue muda mrefu ili kusudi wananchi wote wapate huduma za afya mahali popote watakapoweza kwenda katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma za afya zinazotolewa na Bima ya Afya kwenye hotuba amesema ni asilimia 8 tu ya Watanzania wote na hii nyingine ni asilimia 25 tu. Kwa hiyo, inakuwa haitoshi, kwa hiyo wananchi wengi wanapata shida katika kuweza kupata huduma kwa kutumia Bima za Afya. Pia kuna ahadi kwamba wazee wanaokuwa na zaidi ya miaka 60 watapata matibabu bure. Mipango ya kutoa hivi vitambulisho inakwenda polepole sielewi kwanini kwa sababu katika wilaya yangu hakuna hata mzee mmoja aliyepewa kitambulisho cha kupata matibabu bure na inawezekana na wilaya zingine hali kama hiii na tumeisema kwa muda mrefu. Kwa hiyo naomba sana mharakishe katika mpango huu kuhakikisha wazee wetu kweli wanapata tiba.

Mheshimiwa Mwenyekti, pia nipongeze utaratibu kwamba mna makazi ya wazee wasiojiweza 17. Basi naomba sana yaboreshwe makazi haya na wapate huduma zote ambazo ni za msingi wazee wetu ambao wameta mchango mkubwa sana kwa ujenzi wa Taifa hili. Tusiwaache wanakuwa ombaomba na Serikali yetu sikivu na ina uwezo wa kufanya mambo makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, basi naomba sana suala hili la wazee ulipe umuhimu wa pekee. Pia kwenye hizo hospitali ni kweli liwepo dirisha maalum, wazee wakifika pale wasikilizwe kwanza kabla ya watu wengine. Hili ni jambo ambalo litakuwa jambo jema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja hii na ninakubaliana na mawazo yote ya Waheshimiwa Wabunge kwamba Wizara hii kwa kweli imepata wanaoweza kuleta ufanisi mkubwa. Waziri na Naibu kwa kweli mnafanya kazi nzuri. Mnajibu maswali mazuri, kila mtu huwa anaridhika katika majibu yenu. Nashukuru kwa kupata nafasi. (Makofi)