Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuchangia Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema ambaye ameniwezesha kusimama mbele ya Bunge lako tukufu kuweza kuchangia Wizara hii ya maji. Pili, nimshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya hakika sisi hatuna cha kumlipa ila Mwenyezi Mungu mwenyewe ndiyo atajua cha kumlipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimshukuru kwanza Waziri Mbarawa, Naibu wake Aweso, Katibu Mkuu pamoja na timu nzima kwa kazi kubwa wanayoifanya, kwakweli Watanzania wanaona kazi kubwa mnayoifanya. Endeleeni kufanya hivyo, naamini na Mungu atawasimamia na malengo tutayafikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nishukuru kwa kupewa milioni 500 kwa ajili ya mradi wa Ngulu. Mradi ule umekamilika na sasa nimuombe Waziri au Naibu Waziri aende sasa kwenda kuufungua. Lakini sambamba na hayo, nimepewa milioni 770 kwa ajili ya maji mjini, milioni 770 hizi zimepan giwa zijenge tenki la lita 650 ambalo tenki hilo liko sehemu ya Magamba na tenki lile linaendelea kujengwa mpaka sasa hivi, na banio la sehemu m oja inaitwa Kindoi na banio hilo bado linaendelea kujengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, kwa kuwa kuna kata mbili ambazo ziko chini vyanzo vyake viko juu Lushoto basi nilimuomba Waziri baada ya kufika Waziri Mheshimiwa Prof. Mbarawa baada ya kufika Lushoto kuangalia hali ile halisi ilivyo. Basi nikamuomba kwamba pamoja na kujenga tenki hili, kulijenga, basi kuna banio linajengwa sehemu ya Kindoi niombe banio lile litolewe matoleo mawili kwa ajili ya kata mbili, kwa ajili ya Kata ya Ubiri na Kata ya Ngulwi. Kwa hiyo, niiombe Serikali yangu tukufu kwamba Mheshimiwa Waziri, naomba sasa unipangie fedha au unipe fedha kwa ajili ya kata zile ambazo nimeshazitaja hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hayo, hili tenki la lita 650 naishukuru sana Serikali lakini hakuna mabomba ambayo yanatakiwa kuanza kwenye chanzo kuja kwenye tenki na kutoka kwenye tenki, kwenda Lushoto mjini. Kwa hiyo, niiombe Serikali yangu sasa kwamba pamoja na kupata fedha hizi lakini bado hakuna fedha za miundombinu ya bomba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali yangu initengee fedha hizo ili tuweze kukamilisha miundombinu ya bomba. Sambamba na hayo, miundombinu ya bomba ambayo iko Lushoto Mjini ni ya zamani sana, ni ya tangu mkoloni. Bomba zile ni za chuma Mheshimiwa Waziri. Kwa hiyo, nikuombe sasa unitengee pesa nyingine kwa ajili ya kutoa miundombinu ile ya zamani ili tutoe miundombinu chakavu, tuweke miundombinu mipya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia pamoja na banio hilo niombe sasa kwamba nipate fedha kwa ajili ya kupeleka maeneo yale ambayo nimeyataja kata zile mbili ambazo ni Ubiri na Ngulwi maana nikikosa kwenye eneo hili basi ujue kabisa kwamba wale watu wa Ngulwi na Ubiri hawataweza kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe tena, nimuombe Mheshimiwa Waziri kwamba kuna mradi mkubwa ambao umeshafanyiwa upembuzi yakinifu. Mradi huo unaitwa chanzo cha wanaitwa mstari namba tisa ambao uko Magamba. Chanzo kile kikienda kutekelezwa kitaenda kutatua tatizo la maji katika kata 12 ambazo kata hizo ni Kata ya Makanya, Mbwehi, Malibwi, Kwekanga, Kwahi, Migambo, Kilole, Gare, Ngwelo, Ubiri, Ngulwi pamoja na Kata na Kwemashao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyojua Lushoto, jiografia yake ni ya milima kwa hiyo vyanzo vya maji viko Lushoto. Sisi tumekosa miundombinu ya maji na maeneo haya ina maana yako mlimani, vyanzo viko mlimani, maeneo yako bondeni. Kwa hiyo, kwenye maeneo haya niliyotaja nikipata miradi miwili tu basi ina maana tunaenda kutatua tatizo kubwa katika kata ile. Cha kushangaza na cha kusikitisha, wenzangu wanaongelea vijiji havina maji lakini mimi naongelea kata hazina maji, hebu angalia distance iliyopo hapo. Nimuombe Waziri aliangalie hili kwa jicho la huruma ili niweze kuongelea vijiji, sio kata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Waziri anafahamu kabisa Lushoto na Waziri mwenyewe Mheshimiwa Prof. Mbarawa anafahamu Lushoto. Lushoto kule wananchi wanapata taabu sana hasa katika Kata ya Kwai, Makanya, Malibwi, Mbwehi, Kilole, Kwekanga wananchi wanapata taabu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata mistari ya dini inasema kullukum rai wakullukum masuul. Hii ni dhamana, viongozi tutakwenda kuulizwa juu ya jinsi tunavyolinda mali zetu au tunavyowaongoza wananchi wetu. Kwa hiyo, sisi tusije tukawa masiula, Mheshimiwa Waziri usije ukawa Masiula, Naibu Waziri usije ukawa Masiula. Hakika, wewe Mheshimiwa Naibu Waziri unafahamu Lushoto. Dada zetu wanapata tabu sana, wanatoka mpaka vipara, hakuna hata wa kuwaoa angel face hazikai usoni, carolite hazikai usoni hata lipstick hazikai mdomoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe usije ukawa masiula, hebu angalia suala hili kwa makini, tusije tukaulizwa na Mwenyezi Mungu kwamba umewatendea nini wananchi wa Lushoto hususan akina mama. Nikuom be upeleke fedha katika Jimbo la Lushoto na maene haya niliyoyataja ili wananchi wangu hususan akina mama tuanze kuwatua ndoo kichwani kuliko ilivyokuwa sasa hali ni m baya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, pia niende kwenye suala la kujenga mabwawa. Kama walivyosema, Lushoto ni ya milima milima lakini laiti Serikali ingekuja na mpango wa kujenga mabwawa naamini tusingepata taabu ya maji. Lushoto kuna maji ya mserereko, kwa hiyo, niiombe Serikali sasa itenge fedha kwa ajili ya kujenga mabwawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hayo, waati tunasubiri miradi mikubwa, hebu sasa tupatieni fedha za kuchimba visima virefu ili wananchi wale waanze kupata maji, wananchi wale wasipate taabu san a na ukizingatia sasa hivi wananchi wetu wanatoka asubuhi hususan akina mama. Wanatoka asubuhi saa kumi na mbili wanarudi saa saba. Hivi hawa watoto watawahudumiaje kwenda shule? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Waziri na timu yake iliangalie ili kwa jicho la huruma. Nimeongea sana kwa muda mrefu hususan katika Bunge hili kuhusu mambo ya maji. Kwa kweli kama tumedhamiri akumtua mama ndoo kichwani basi kweli tumtue mama ndoo kichwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, watumishi Wizara ya maji mpaka kule chini kwenye idara hawatoshi ni wachache sana ndiyo maana unakuta mambo yanazorota. Pamoja na hayo, kuna hii sheria ya manunuzi, hii sheria inakandamiza sana na ndiyo inapelekea miradi inakuwa miradi inatengwa kwa gharama kubwa sana. Mfano unaweza ukaona get valve ya inchi sita inauzwa 1,000,000…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa, muda wetu ndiyo huo.

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)