Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kushukuru kipekee kabisa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wabunge wote ambao walikuja kuniona nilipokuwa nimelazwa pale Hospitali ya Muhimbili, nasema ahsante sana wote mliokuja na ambao hamkuja wote mlifanya kazi moja ya kuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache tu ambayo ninataka kuchangia ni Mradi wa Matamba na Kinyika, Wilaya ya Makete ambao Wizara imeandika barua ya kwamba kupewa no objection. Mpaka sasa hivi hatujapewa no objection na mradi huu ni wa bilioni 4.6, ni vizuri Mheshimiwa Waziri akaupa no objection mradi huu ili mambo yaende mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi mwingine ni wa Bulongwa ambao unajumuisha Bulongwa, Iniho, Kapagalo, Usililo, nayo ni umeshakamilika unahitaji milioni 264, lakini huyu mtu amemaliza kufanya kazi hiyo, fedha hajapewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi mwingine ni Mradi wa Lupalilo- Tandala ambapo zinahitajika milioni 161, mpaka sasa hivi bado hajapewa, naomba sana Mheshimiwa Waziri ukumbuke kufanya jambo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi mwingine ni Mradi wa Igumbilo ambao ni milioni 308 zinahitajika ili ziweze kutekeleza mradi huo, naomba sana sana Wizara iweze kutoa fedha hizo ili mradi uweze kutekelezeka. Zaidi ya hapo nipongeze sana sana Serikali ya CCM, Mheshimiwa Waziri Profesa Mbarawa, Katibu Mkuu Profesa Kitila Mkumbo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwezesha miradi hii kutekelezeka. Mungu awabariki sana. Ahsante sana. (Makofi)