Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Awali ya yote nami nianze kumshukuru Waziri Mheshimiwa Mbarawa, nafahamu aliweza kututembelea Mkoa wa Katavi na kwa pamoja tulikwenda kwenye chanzo cha Ikolongo lakini alifuatilia suala la Bwawa la Milala na akaona hali ya ugawaji maji katika Mji wetu wa Mpanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu umuhimu wa maji kama walivyozungumza wazungumzaji wengine waliotangulia na kwa kuanzia nikiwa nimetangulia na kuunga mkono hoja, naomba niliweke katika sura zifuatazo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kugawa fedha I mean ile Sh.50 tunayoiomba sina matatizo nayo, rai na ombi langu tunapokuwa na pipa lenye tundu wakati tunaendelea kujaza maji kwenye pipa hilo, ufumbuzi ni kwenda kuziba tundu, vinginevyo tutaendelea kuhakikisha pipa lile halijai maji. Kwa hiyo kupewa fedha, kuwaombea fedha sina tatizo nalo, lakini kudhibiti matumizi ya fedha hapo ndipo ilipo hoja ya msingi.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka hapo, naomba, nafahamu kwa maana ya Jimbo langu la Mpanda Mjini tulipatiwa visima 15, uungwana unanituma kushukuru na visima vile vilishafanyiwa pumptaste, jambo linakwenda vzuri. Lililobaki Mheshimiwa Waziri na wananchi wale wamesharidhika na kazi nzuri ya Serikali kama tumefikia hatua hii ya pump taste limebaki jambo moja tu la kufunga pump. Kwa hiyo niiombe Wizara tukamilishe zoezi hilo la kufunga pump ili wananchi wale waendelee kuwa na imani na Serikali yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukikamilisha suala hilo la ufungaji wa pump kwa visima 15, naomba nishukuru tena, nafahamu tumesaini kwa maana ya Ikolongo namba mbili na Mheshimiwa Waziri tulikwenda pamoja akakiona chanzo kile, Mji wetu wa Mpanda asilimia ya maji ambayo inagawanywa pale ni kati ya asilimia 30 ambayo ni kiwango kidogo na ukienda field inaweza ikawa chini ya asilimia 30, tuna maeneo ya Makanyagio, tuna maeneo ya Majengo kwa ujumla pale mjini kati mgawanyo wa maji ni tatizo na tunapata matatizo wakati vyanzo vimetuzunguka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba Serikali wametusaidia kwa maana ya kusaini na Wakandarasi wako site kwa maana ya Ikolongo namba mbili. Ninachokiombna fedha zile za awali zimetolewa lakini naomba basi ili tukiusukuma huo mradi wa Ikolongo namba mbili tatizo la maji kwenye eneo letu la Mji wa Mpanda itakuwa historia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kupongeza zaidi, najua tunakwenda kuusubiri mradi mkubwa kuyatoa maji Ziwa Tanganyika kuyaleta maeneo ya Mpanda na kwingineko. Najua mradi huu utakuwa ni mwarobaini wa matatizo ya maji katika maeneo yetu. Wakati tukiishi kwa matumaini kwa mradi huo, nilichokuwa nakiomba sana Ikorongo Namba Mbili itakuwa ni ufumbuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua pia tuna mradi mmoja wa Manga – Kasokola, toka tumeleta certificate katika Wizara, ililetwa tarehe 12 Desemba, 2018 ya shilingi milioni 47 mpaka leo haijalipwa. Mradi ule kwa maana ya Manga na Kasokola, mkandarasi amefika sehemu ya kukata tamaa. Nachokiomba, tukipatiwa fedha hizi akalipwa mkandarasi sehemu ile ya Vijiji vya Manga na Kasokola tatizo la maji nalo litakuwa ni historia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona maeneo mengine wakizungumzia kuhusu vyanzo vya maji kwa maana ya mabwawa; sisi katika Mji wetu wa Mpanda tunalo Bwawa la Milala. Ni bwawa zuri lakini tatizo chanzo kile kama kimetelekezwa fulani hivi. Viboko wamezaliana, maji ni machafu, wakati wengine wanahangaika tutapata wapi maji sisi chanzo tunacho tatizo ni utunzaji na kuhakikisha tunaya-treat yale maji ili kuongeza mserereko wa maji pale Mpanda Mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wanalalamika watapata wapi maji, sisi maji tunayo chanzo kipo cha Milala. Historia itatuhukumu kama watu walifanya kazi nzuri kuhakikisha chanzo kile kimekuwepo leo chanzo kipo tunakitelekeza kwa makusudi. Naomba Wizara ikiangalie chanzo hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati mbaya sana Bwawa la Milala limekuwa ni mazalio ya viboko limeanza kuwa ni hatari hata kwa wananchi wa Mpanda. Tuna Shule ya Mpanda Girls pale, viboko wale usiku na shule haina uzio ni hatari lakini wamekuwa wakitoka pale bwawani wanakuja mpaka Mjini Mpanda kuharibu mashamba ya watu lakini limekuwa pia ni tatizo kwa maana ya usalama wa wananchi wetu. Naomba hilo nalo mliangalie kwa namna ya pekee. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)