Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niseme maneno machache sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, naunga mkono hoja. Pili, nitoe pongezi kwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu nzima kwa jinsi wanavyofanya kazi, wanafanya kazi vizuri. Tunaelewa kwamba wameikuta Wizara ina changamoto mbalimbali lakini wanaendelea kupambana nazo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo napenda kulikumbusha, tulipoingia Bungeni baada ya muda kidogo tuliwekewa fomu kwenye maboksi yetu pale tukaambiwa tuandike miradi yenye matatizo. Sasa kwangu iko miradi yenye matatizo na niliandika na haijachukuliwa hatua. Juzi alipokuja Mheshimiwa Makamu wa Rais, tulikuwa na Naibu Waziri, mradi wa Nyahau ulileta shida kidogo lakini Mbunge alikwishawasilisha. Mimi niliomba miradi yangu hiyo yote ifanyiwe audit na nilikuwa na maana yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka miradi ya Iguguno, Kikonda, Kidarafa na Mtamba ifanyiwe audit kwa sababu design na kilichojengwa siyo chenyewe. Tulikwenda na Waziri aliyeondoka mwananchi wa kawaida anasema tuliambiwa ma-tank mawili na visima vya kuchotea maji kadhaa. Kwa hiyo, mwananchi wa kawaida anazo data, mainjinia wetu kwa nini hizo data hawazifanyii kazi. Bado nasisitiza tunaomba miradi hiyo ifanyiwe audit lakini pia hiyo liability nimeshaihamishia Wizarani kwamba nimesema ziko changamoto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, Waziri alipofika Kidarafa na Kikonda aliahidi solar. Mheshimiwa Waziri nilizungumza, nafikiri jambo hilo linafanyiwa kazi maana kuendesha miradi hiyo kwa kutumia diesel ni gharama kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitabu nimesoma, ukurasa wa 167 kuna shilingi milioni 90 zimetengwa naomba ule mradi usome Lelembo. Kwa heshima kubwa Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Waziri naomba mradi huu usomeke Lelembo. Nikisema kwa heshima kubwa nina maana yangu na nina maana kubwa sana na ikibidi tuma wataalam wako wachunguze kwa nini nimesema hivyo na jambo hili nimezungumza na Mkurugenzi. Kwa hiyo, tumekubaliana pasomeke Lelembo, mradi ule uende ukakamilike na huu ni mradi mmojawapo yapo majenereta mapya kabisa pale yanaoza, naomba mkayachukue muondoke nayo, maana siyahitaji lakini najua watu wengine watahitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nizungumzie kuhusu malipo ya wakandarasi. Certificate za wakandarasi hazijalipwa miradi wa Nduguti, Kinyangiri na Ipuli, tunaomba waweze kulipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na mradi wa visima 10, kihistoria tuna vijiji 70 lakini vijiji ambavyo vina maji havifiki 10 isipokuwa ule mradi wa vijiji 10 ungefanya vijiji 20 viwe na maji. Tunaomba hiyo miradi basi itengewe fedha kidogo kidogo lakini pia tunaomba usimamizi, jicho la karibu muweze kuona utekelezaji wake unakwenda vipi. Hizi fedha mnazoweka huko na siasa za kwenye Halmashauri huko unakuta fedha zinakuwa diverted zinakwenda kufanya miradi mingine tena. Kwa hiyo, tuna miradi lakini inaanzishwa mingine, kwa hiyo, tunaomba jambo hilo liweze kuangaliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, usimamizi wa miradi. Wilaya nyingi mpya zina changamoto ya magari, tunaomba hata gari bovu sisi tutatengeneza. Yaani gari lile bovu kabisa lililoko Wizarani nyie mtupe, mimi niondoke nalo Bunge likiisha, halafu tutakwenda kulitengeneza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko jambo lingine ambalo tulikuwa tukizungumza la vyanzo vya maji. Yako maji mengi wamezungumza Wabunge wengine ambayo yanatiririka. Kwenye Bonde lile la Msingi maji yanatiririka mpaka Nyahaa kule. Niliwahi kuuliza swali hapa la msingi kwamba utafiti unafanyika, hakuna namna ya kukinga yale maji? Kwa sababu sisi hatuna ile mito inayotiririka kwa mwaka mzima ili tuweze kupata maji, sasa hilo bonde likifanyiwa tathmini tunaweza tukapata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine kwenye visima vilevile 10 tunaomba mtume auditor, visima vimechimbwa, watu wamelipwa wameondoka vingine havina maji na fedha ya Serikali imeshakwenda. Hilo ni jambo la muhimu sana la kuweza kuangalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wamezungumzia suala la Force Account. Ni muhimu sana tukaangalia kama kuna uwezekano tukaenda kwa approach hiyo tunaweza tukaokoa fedha nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tulianzisha Mfuko wa Maji, wamezungumza Wabunge wengi, lazima tukubaliane kwamba unahitaji fedha na kama unahitaji fedha tunafanya nini. Sasa tukubaliane kama Bunge hapa, tuangalie chanzo mahali popote pale, fedha ya Mfuko ya Maji iende, kile kiwango tukiongeze ili tuwe na fedha nyingi kwenye Mfuko wa Maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwa na fedha nyingi kwenye Mfuko wa Maji hizo fedha basi na zenyewe zionekane vijijini. Wamesema wenzangu hapa mijini wana miradi mingi ya wafadhili lakini vijijini watu wanahitaji maji. Kauli kubwa hapa watu wanayozungumza, kila mtu anazungumza suala la maji. Leo sijazungumzia asilimia ya upatikanaji wa maji vijijini kwa sababu wenzangu wameshazungumza. Tufikie mahali tuwe na takwimu sahihi ya upatikanaji wa maji vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii fupi. Ahsante. (Makofi)