Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa nafasi hii ya kuchangia kwa maandishi. Tunaishukuru sana Serikali kwa kutuletea zaidi ya shilingi milioni 400 kwa ajii ya kuboresha miundombinu ya shule za msingi. Tumeweza kuboresha shule za msingi kadhaa zilikiwemo Shule ya Msingi ya Kisesa, Shule ya Msingi ya Mwakipanga, Shule ya Msingi ya Chipukizi Mjini ya Igunga na shule nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashukuru pia kwa Serikali kutuletea zaidi ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Shule za Zekondari Nanga, Bukoko, Igunga na nyingine. Bado changamoto ni nyingi, tumeleta maombi ya kuanzisha shule za high school mbili; Shule ya Sekondari ya Bukoko kwa ajili ya wasichana na Shule ya Sekondari ya Igurubi kwa ajili ya walemavu. Je, Wizara imeliingiza ombi letu hili kwenye bajeti hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru tena kwa fursa hii.