Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natoa pongezi kwa Serikali kwa kuendelea kuimarisha elimu nchini. Pongezi kwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Maendeleo Msaginya (Katavi) ni muhimu sana kwa kuelimisha vijana katika sekta mbalimbali kuanzia watoto wenye elimu ya msingi. Chuo hiki kimepata ajali ya kuungua moto mara mbili ndani ya mwaka mmoja. Hivyo, tunaomba Serikali kupitia Wizara kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili kwa kuwa watoto wanaishi katika mazingira magumu sana. Hivyo, tunaomba uwezeshaji ufanyike kwa haraka. Uongozi wa chuo umeshaleta barua Wizarani kwa taarifa na utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania imekuwa kinara katika kutoa elimu isiyo na mfumo rasmi (non-formal education). Tunayo UPE na Elimu ya Watu Wazima na nyinginezo, napenda kupata maoni ya Serikali, je, mpango upi uliopo wa kuboresha elimu hii? Pia Serikali imetenga kiasi gani kwa ajili ya mfumo huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Teachers’ Professional imepitishwa lakini bado inahitaji maboresho yafuatayo: Moja, uteuzi wa regional and district representative. Katika sheria uteuzi unafanywa na Waziri wa Elimu. Nashauri uteuzi ufanywe na registrar kwa kushirikiana na bodi. Pili, Teachers’ Professional haina mamlaka ya kuhakiki walimu na taaluma zao, hivyo mitaala iwe inapitiwa na Bodi ya Teachers’ Professional ili kuhakikisha wahitimu ni watu wenye sifa zinazotakiwa, kama professional bodies nyingine zinavyofanya, mfano Uhasibu, Sheria (Law School) na Manunuzi. Tatu, utunzi wa kanuni uzingatiwe kwa wakati ili kuharakisha utekelezaji wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaomba Serikali iendelee kukarabati shule kongwe za msingi katika Halmashauri ya Nsimbo; Songambele, Isinde, Ikolongo, Katambike, Mtapenda, Isanjandugu na Uruwira.