Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Spika, naomba nichukue fursa hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo kwa kunipa afya njema hata kupata fursa ya kuchangia.

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anafanya na pia wasaidizi wake wote. Nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu pamoja na viongozi wote wa Wizara na Taasisi zake zote kwa kazi kubwa na nzuri wanayofanya katika kuboresha Sekta ya Elimu.

Mheshimiwa Spika, naomba nichangie katika maeneo machache katika kuboresha sekta hii. Kwanza naomba kuishauri Serikali kurejesha upitiaji wa Sheria ya Skills Development Levy (SDL) ya asilimia mbili ya SDL iliyopelekwa Bodi ya Mikopo mwaka 2014 kwa dharura. Muda sasa umefika kurejesha hiyo asilimia mbili iende kuboresha taasisi zetu za ufundi. Kwa hali yetu ya uchumi na tunakoelekea, hasa kwa sera yetu ya viwanda na uhitaji wa wataalam katika viwanda (technicians) na pia ujuzi katika maeneo mbalimbali ambayo yatatoa fursa kubwa za ajira badala ya Watanzania wengi kwenda katika elimu ya ajira ya utawala na usimamizi tu (white collar jobs), tuboreshe shule zetu za ufundi, vyuo vya ufundi na pia kuwa na mfumo kuanzia sekondari ya kufundisha ujuzi mbalimbali ili tuweze kujiajiri.

Mheshimiwa Spika, pili, katika sayansi na technolojia, naomba Serikali iweke bajeti ya kutosha; na pendekezo lilikuwa kwa asilimia moja ya bajeti yetu. Nchi haiwezi kwenda bila sayansi na teknolojia. Bajeti inayopelekwa katika utafiti ni ndogo sana. Bajeti yote haikidhi hata haja ya kituo kimoja ya utafiti. COSTECH iwezeshwe zaidi, kwani ndiyo chanzo kikubwa na pekee nchini kinachoratibu masuala ya utafiti. Fedha zile shilingi tano kwa unit ya TTMS zirudishwe. COSTECH walikosa baada ya Wizara kuwa na muundo tofauti. Ni chanzo cha uhakika cha mapato kwa ajili ya kuboresha utafiti.