Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mchango wangu wa jana, napenda kuongeza kwa haya yafuatayo kwa maslahi ya Mkoa wetu wa Rukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Rukwa tunayo maboma kadhaa na majengo ya nyumba za walimu, madarasa, vyoo na maabara jumla ni 208 lakini kati yake maboma 177 ya maabara bado hayajakamilika na kupelekea wasiwasi wa kupata mafunzo kamilifu ya sayansi kwa watoto wetu. Tunaomba Mkoa wa Rukwa utizamwe kwa jicho la pekee hasa mkizingatia tupo pembezoni nasi tulichelewa katika suala zima la elimu, tumekuja kuibukia hivi sasa. Tunaomba fedha iliyoandaliwa kuhusu ukamilishaji wa maboma ya majengo ya elimu, Mkoa wa Rukwa tuwemo katika mgao wa fedha hizo kwa zaidi ya nusu ya maboma hayo ya maabara kwa makusudi maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyozungumzia kuhusu matatizo ya kiwango cha pesa zitolewazo kwa ajili ya chakula kwa shule zenye wanafunzi wenye mahitaji maalum, kwa shule zetu za Mkoa wa Rukwa, tunazo pale Kata za Ndala B, Mwenge A na Malangali kwa mwaka fedha zinazotolewa na Serikali ni kiasi cha shilingi bilioni 22 wakati mahitaji halisi ni shilingi bilioni 72.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachohitaji kuongezea hapa ni usalama wa shule hizi hasa Shule ya Walemavu Malangali. Malangali ni shule ya bweni lakini haina uzio na watoto ambao ni wenye ualbino wanakuwa katika wasiwasi wa maisha yao na hata walimu wao wanakuwa na kazi ya ziada ya ulinzi wa watoto hao. Tunaomba Serikali ione umuhimu wa ujenzi wa uzio wa shule hiyo kwani ni shule inayosaidia na mikoa ya jirani na wakati wa likizo wengi wao hawaendi majumbani kwa kuhofia usalama wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuweka msisitizo kuhusu Chuo cha FDC - Chala kwa kuwa majengo hayo yanahitajika kurejea kwenye umiliki wa Askofu wa Kanisa la Katoliki, ingawa miundombinu yake imechakaa kwa kiasi kikubwa sana, wananchi wametoa eneo na majengo kadhaa yameanzishwa kwa nguvu za wananchi. Kwa kuzingatia na kuheshimu mchango wa wananchi wetu, tunaomba mgao wa fedha hizo za kukarabati Vyuo vya FDC kwa Mkoa wa Rukwa zielekezwe kwenye eneo hili tukamilishe Chuo chetu cha FDC mbadala wa Chuo cha FDC – Chala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.