Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Naibu wake kwa utumishi wao wa unyenyekevu, kujituma na usikivu katika kutekeleza majukumu yao. Nimpongeze sana pia Mheshimiwa Rais kwa kutoa kipaumbele cha juu kabisa kwenye suala la elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa Mheshimiwa Waziri kunitengea fedha za kukarabati upya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi cha Malampaka. Naomba sasa ramani za majengo yatakayokarabatiwa zipelekwe kwenye Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Malampaka ili ujenzi na ukarabati uanze mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshasubiria kwa muda mrefu sasa ramani hizi hazikamiliki na sababu ya kweli ya kuchelewesha ramani hizi bado haijajulikana. Naomba sana mchakato huu uharakishwe ili ukarabati wa chuo hiki uweze kuanza na hatimaye kuwafaidisha wananchi wa Maswa na Jimbo la Maswa Magharibi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.