Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri, Prof. Ndalichako pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri, Olenasha kwa kazi nzuri wanayoifanya katika sekta ya elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi zangu, naomba sana Mheshimiwa Waziri aendelee kupigania elimu bora katika nchi hii. Mwaka juzi kuna baadhi ya shule za Serikali na shule binafsi zilipata kashfa ya udanganyifu wa mitihani, hili ni jambo baya wala halikubaliki. Pamoja na adhabu mlizochukua ikiwa ni kufutia mitihani na kuzifungia shule hizo, naomba sana adhabu hizi zisiweze double standard kwa kuziadhibu shule binafsi na kuziacha shule za Serikali wakati kosa ni lile lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule za binafsi zimenyimwa nafasi ya wanafunzi wao kufanyia mitihani katika shule zao, wamebadilishiwa centre za mitihani pamoja na kuendelea kuwafundisha wanafunzi katika shule zao na mbaya zaidi hata matokeo yakitoka yanalenga katika shule walizofanyia mitihani. Ombi langu adhabu iwe common kwa yeyote atakayefanya kosa, kubagua ni dhambi. Naomba kuchukua fursa hii kuwaombea msamaha wenye shule za binafsi kwa muda wote huu watakuwa wamejifunza kosa lao na hawatakuwa tayari kulirudia tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja, Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri endeleeni kuchapa kazi.