Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia kuhusu kuboresha maslahi ya walimu. Suala hili la kuboresha maslahi ya walimu wetu ni muhimu ili kuleta morali kwa walimu na matokeo chanya kwa watoto na hasa kizazi hiki ambacho kinakabiliwa na kuzungukwa na utandawazi ambao unawaathiri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri mitaala yetu iendane na teknolojia yetu. Kutokana na suala la teknolojia kubadilika kila wakati hivyo mitaala yetu ni vyema kuzingatia mabadiliko hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lugha za alama kwa wanafunzi wenye ulemavu. Wanafunzi hawa wanahitaji kupata elimu kama wanafunzi wengine ili kuleta usawa na kuondoa malalamiko miongoni mwa wanafunzi ambao wako kwenye jamii zetu zinazotuzunguka. Kwa hiyo, ni muhimu lugha hizi ziwepo katika shule zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuna upungufu wa walimu wa lugha za alama. Nashauri ili kumaliza tatizo hili Serikali iongeze vyuo maalum kwa ajili ya walimu wa lugha za alama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushirikishwaji wa wadau wa elimu wanapotaka kufanya mabadiliko katika masuala ya elimu. Kumekuwa na matokeo hasi kwenye maamuzi mbalimbali yaliyotokea katika masuala ya elimu sababu kubwa ni kutowashirikisha kikamilifu wadau wa elimu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mafunzo maalum kwa walimu. Kulingana na mabadiliko yanayojitokeza kwenye elimu ni vyema walimu wetu wakawa wanapewa mafunzo ya mara kwa mara ili kuboresha elimu yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyuo vya ufundi. Bado kuna upungufu mkubwa wa vyuo vya ufundi nchini kulingana na wahitimu wa ngazi mbalimbali kuwepo mitaani lakini hata vile vichache vilivyopo vina changamoto za walimu kuwa wachache pia hawapelekwi kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuongeza pesa kwenye suala la ukaguzi kwa kuwa matokeo chanya ya elimu yatatokana na ukaguzi. Nashauri Serikali ili kuboresha elimu yetu ni vyema kuboresha Kitengo cha Ukaguzi pia Wizara ishughulikie kero zinazotokana na ukaguzi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Elimu ina mkanganyiko sana. Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza sera hizi ambazo zimekuwa na mkanganyiko mkubwa?