Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo ya wanafunzi bado ni tatizo, kwanza inachelewa na pili inatolewa bila kufuata taratibu. Mfano, kuna yatima ambao wamejaza vizuri pamoja na yote hayo bado hawapewi mkopo wanapewa ambao wana uwezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, motisha kwa walimu. Hakuna elimu bora bila walimu kupewa motisha. Hata kama mna madarasa mazuri kiasi gani au miundombinu yote iwepo bila kuhakikisha walimu wana ari ya kufundisha ni kazi bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukataji mikopo kwa asilimia 15. Tukumbuke kuwa wapo pia walimu ambao wanakatwa mikopo na mshahara yao ni midogo. Ukikata mkopo kwa asilimia hizo unamwacha hana chochote na kushindwa kuwajibika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bure. Changamoto za elimu bure ni kubwa mno, watoto ni wengi, hakuna madarasa, walimu, vifaa vya kufundishia na maabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria za uanzishaji shule. Shule za Serikali zinaanzishwa hata kama hakuna vyoo, madarasa machache ukilinganisha na za binafsi ambazo unakuta hazipati usajili wakati pengine hawana baadhi ya mahitaji madogo tu. Tuangalie na kuwatia moyo wenye shule binafsi kwani wanaisaidia Serikali kielimu hivyo inatakiwa sekta binafsi hii isaidiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti kushuka. Naomba tuangalie suala hili maana watoto ni wengi madarasani wakati fedha zao haziongezeki, mishahara haiongezwi, hakuna mafunzo ya ziada ya mitaala na sera zinabadilishwa lakini walimu hawapati mafunzo juu ya mabadiliko hayo.