Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa ya kuchangia kwa maandishi kama ulivyonipatia hapo awali fursa ya kuchangia moja kwa moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kwa usimamizi mzuri wa Serikali. Pia naendelea kuipongeza Wizara kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Magu, Kata ya Bujora kuna Shule ya Sekondari ya Lunve. Shule hii imekuwa mkombozi mkubwa kwa wanabujora kwani wanafunzi walikuwa wanatembea umbali mrefu kutafuta elimu toka shule za kata za jirani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa mchango wake katika ujenzi wa shule hiyo japo bado kuna mahitaji makubwa na ni hivi karibuni tumepokea shilingi milioni 25 kwa ajili ya madarasa mawili (2). Shule ina majengo sita tu yaliyokamilika huku wananchi wakiendelea kujenga madarasa manne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shule haina madawati ya kutosha na wanafunzi wanakaa chini na matundu ya vyoo ni machache kulingana na mahitaji. Naomba sasa Wizara iweze kuiangalia shule hii kwa jicho la tatu ili ipate uwezesho katika mwaka wa fedha ujao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja.