Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kuongelea changamoto zinazowakabili watu wenye mahitaji maalum (viziwi). Kumekuwa na changamoto kubwa sana kwa wenzetu hasa soko la ajira haliwapi fursa kuweza kupata nafasi za kazi na fursa za kujiajiri; ushauri wangu Serikali iangalie mitaala maalum itakayoweza kuwapa wenzetu hawa fursa ya kuingia kwenye soko la ajira ili waweze kuona tija ya elimu wanayopatiwa.

Masomo ya dini (Bible knowledge na Islamic religion) kupatiwa thamani kwenye ufaulu wa wanafunzi; Serikali imekuwa ikilipa mishahara kwa walimu wanaosomesha masomo ya dini shuleni na pia Serikali imekuwa ikiingia gharama kuandaa mitihani kwa masomo hayo bila ya kupatiwa thamani kwenye ufaulu. Kwa vile kila mwanafunzi anatarajiwa kuwa muajiriwa mtarajiwa na kwa kila mwajiriwa anahitaji miongozo ya kiroho, Wizara sasa ina haja ya kuona namna ya kuipa thamani masomo haya kwenye ufaulu wa wanafunzi.