Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Kamishna wakuu wa Idara na wafanyakazi wote kwa kazi nzuri na ngumu mnayofanya. Kwa niaba ya wananchi wa Urambo pokeeni shukrani za dhati kwa kukubali kuanzisha Chuo cha VETA Urambo asante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ombi tunaomba sana Chuo hicho kiwe na miundombinu hususan Karakana ili wapate ufundi wa aina mbalimbali pamoja na mafunzo yote mafunzo ya udereva (Driving) isikosekane kwa kuwa hakuna Urambo inabidi waende Tabora. Hakika ndoto yetu ya kuwa na VETA imetimia. Watoto wa kike watapata mahali pa kukua baada ya kumaliza masomo wakiwa na umri mdogo, Mwenyezi Mungu awabariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba pia mabweni hasa kwa high schools za Vyumbu na Urambo. Tutashukuru sana mkituruhusu tuongeze shule mbili za high school za Ukondamoyo na Usoji. Tutaleta maombi karibuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali, je, Serikali haioni umuhimu wa kuagiza kwamba shule mpya inapojengwa ianze na vyoo kwa kuwa madarasa yanapojengwa wa fedha huisha na kushindwa kujenga vyoo bora na vya kutosha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri. Pamoja na kwamba mabweni si utatuzi pekee wa suala la mimba shuleni lakini linachangia kwa kiasi kikubwa. Ni vyema kukawa na mkakati wa kujenga mabweni kama ilivyo kuwa maabara na madawati. Nawatakia kila la heri kazini.