Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Manaibu Katibu Wakuu pamoja na watumishi wote wa wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuipongeza Wizara kwa maboresho ya utendaji wa kazi hususani katika maeneo yote yanayohusu elimu, hii ni pamoja na Taasisi zote za Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya maneo muhimu yanayochangia ufaulu ni pamoja na kuwa na Maktaba za kisasa zenye vitabu. Nalisema hili kwa kutolea mfano wa maktaba ya kisasa iliyojengwa kwa ufadhili wa nchi hisani ya China katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hakika naipongeza Nchi ya China na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyakiti, nashauri sana kuwa na maktaba kama ile katika vyuo vyote. Najua ni gharama lakini katika elimu huwezi kuepuka suala la gharama. Tuanze kidogo kidogo katika vyuo vyote hii itasaidia sana kuzalisha wataalam wazuri na kuimarisha elimu yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niishukuru Serikali kwa kutupatia Gari kwa ajili ya udhibiti wa elimu katika jimbo langu kwani Jimbo la Kilindi ni miongoni mwa maeneo yenye changamoto sana kwa sababu ya ukubwa wake lakini miundombinu isiyoridhisha. Pamoja na kutupatia Gari tunayo changamoto kubwa nayo ni kukosa Dereva lakini hatuna kasma ya matengenezo ya Magari na mafuta pia kwa maana kifungu cha mafuta hakipo. Niishauri sana Serikali, ili tija ipatikane ya uwepo wa chombo hiki pamoja na stahiki za watumishi na eneo hili. Aidha, hatuna jengo kwa ajili ya watumishi, tunalo eneo naiomba sana Serikali itujengee Ofisi za Watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nipongeze juhudi za Serikali katika kuhakikisha ujenzi wa vyuo vya VETA katika ngazi za Mikoa na pia katika ngazi za wilaya. Vituo hivi vitatoa tija kwa vijana wetu katika kutatua changamoto ya ajira kutoa ufundi mbalimbali lakini dhima ya viwanda vya kati haitofanyiwa bila kujenga VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ukurasa wa 43 wa hotuba yako kipengele (vii) nimeona jitihada za Serikali za maandalizi ya michoro na zabuni kwa ajili ya ujenzi wa vyuo viwili vua ufundi stadi vya Wilaya ya Kilindi na Karagwe. Hili jambo kubwa sana Kilindi wanasubiri ujenzi wa VETA kwa hamu kubwa sana kwani ni miongoni mwa maeneo ambayo yana vijana wengi ambao hawabahatiki kuendelea na masomo lakini ni miongoni mwa maeneo yenye fursa za madini, jamii ya wafugaji pia hivyo kupata chuo cha VETA kitasaidia sana vijana wetu. Niiombe sana Serikali iongeze jitihada za ujenzi kama inavyoahidi hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.