Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Mikopo; ni jambo lenye tija kuunganisha taarifa za Bodi ya Mikopo na TASAF, ili kuondoa utata au usumbufu kwa walengwa wakati wa uombaji wa mikopo hiyo. Kwa kuwa watu wanaohudumiwa na TASAF wanakuwa na namba, ni muhimu wapewe namba na barua ya kuwatambulisha wakati wa kuomba mikopo ili kuondoa utata huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la kutoa ushauri huu ni kuwa kuna wengine hufiwa na wazazi wao na kisha hupata kibali cha kifo. Kwa hiyo basi, ni vyema kibali cha kifo kitambulike wakati taratibu nyingine za kufuatilia cheti zinafanyiwa kazi kwani elimu ni haki ya kila mtoto wa kitanzania.