Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuchangia mambo machache kwenye hoja hii iliyopo mezani, mahususi nikirejea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuanza na hoja ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Bodi hii imeshindwa kutambua wakopaji wake na wako wapi kwa sababu bodi haina mfumo wa kuwatambua ili kupata marejesho yake. Thamani ya deni hilo ni shilingi trilioni 4.6, rejea ripoti ya CAG 2016/2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Elimu imeshindwa ujenzi katika Chuo cha Ualimu cha Ndala licha ya bajeti ya shilingi bilioni 46 kutengwa na wizara. Niombe Serikali ikatekeleze ujenzi wa chuo hicho cha Ndala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa pia kuchangia kuhusu ukaguzi maalum wa Chama cha Walimu (CWT). CAG alifanya ukaguzi maalum CWT na kuanika ubadhilifu mkubwa katika Chama cha Walimu. CWT ilifanya matumizi ya shilingi bilioni 26.8 bila kuzingatia bajeti; pesa hizi zilichepushwa kutoka kwenye matumizi husika na kufanya matumizi mengine. Malipo ya shilingi bilioni 11.5 yalifanyika bila uambatanisho toshelezi. Matumizi hayo hayakuwa na vielelezo kuthibitisha matumizi hayo, hivyo mkaguzi alishindwa kuthibitisha uhalali wa malipo hayo. Malipo ya shilingi bilioni 3.3 yalifanyika bila kuidhinishwa na Katibu Mkuu na mweka hazina wa Chama cha Walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kuzungumzia suala la Tume ya Huduma za Walimu (Fungu 40). Tume hii ilifanya malipo yasiyo ya kawaida, shilingi milioni 721 kulipa posho, overtime na safari hewa.