Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nchi yetu inaingia kuwa Tanzania ya viwanda bado upande wa elimu bajeti inazidi kushuka, sijui Serikali inajipangaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuchukulie suala la Walimu, Walimu ni wachache sana hadi leo hii zipo shule zina Walimu wachache sana ukilinganisha na takwa la elimu. Walimu hao hao wachache hawana maandalizi mazuri ya kufundishia; miundombinu si rafiki, maeneo wanayoishi, madarasa yenyewe na hasa shule za vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madeni ya Walimu wanayoidai Serikali, kupandishwa daraja, nauli za likizo na marupurupu mengine kwa kazi ngumu kama ya Mwalimu kumfundisha mwanafunzi aelewe kile anachojua yeye, halafu haki zake za msingi halipwi, atakuwa na moyo gani wa kufanya kazi hiyo. Naomba Waziri anapokuja kuhitimisha aniambie kwa mwaka wa bajeti 2019/2020 Wizara yake imejipangaje kumaliza madai ya Walimu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua kwa kuwa, kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaomaliza darasa la saba imefikia milioni moja kwa mwaka, wanaochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ni laki tatu tu, laki saba wanabaki , umri wao ni mdogo ni miaka 12 – 14, hawawezi kufanya kazi ya uzalishaji. Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kundi kubwa hili haliishii mitaani, kunakuwa na vyuo vya VETA kila wilaya ili kupunguza ongezeko la wahalifu nchini.