Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema. Namnukuu Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela; “Education is the most powerful weapon which we can use to change our World”

Mheshimiwa Mwenyekiti, maneno haya yanaonesha jinsi gani elimu ilivyo na umuhimu katika maisha ya mwanadamu ya kila siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la uhaba wa madarasa; kufuatia kuongezeka kwa wanafunzi wa shule za msingi kuanzia STD I – STD VII, ufaulu umeongezeka (2019 – 17% primary schools) wanafunzi wameongezeka lakini bajeti inayotengwa haiongezeki. Hali hii imepelekea wanafunzi wa Kidato cha I (Form one) kukosa madarasa ya kutosha na kupelekea wanafunzi wengine kuchelewa kujiunga na masomo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Serikali kupeleka fedha za ujenzi wa madarasa, bado fedha zinahitajika, bajeti iongezwe na Serikali ihakikishe kila mwanafunzi aliyefaulu anaingia darasani, kwa kujenga madarasa ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga ilibahatika wakati wa Ukoloni wa Ujerumani ilijengwa Shule ya kwanza Afrika Mashariki na Kati, shule iliyozalisha pia Walimu waliopelekwa katika nchi jirani, hali iliyopelekea Tanzania kuwa na historia iiyotukuka katika maendeleo ya elimu. Kwa sasa Halmashauri ya Jiji la Tanga inazo shule za Sekondari, High Schools, vyuo lakini hatuna Chuo Kikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru Wizara kutupatia Tsh. 1.8 bilioni kwa ukarabati wa Tanga Technical School, lakini Tanga hakuna Chuo Kikuu cha Serikali. Naomba Serikali yangu iwaeleze wananchi ni lini itajenga Chuo Kikuu Tanga? Kama itakuwa tatizo ni fedha, mwaka jana niliomba kuipandisha Daraja Galanos High School kwa kuwa inazo “facilities” zote na nyongeza kidogo kuwa Chuo Kikuu. Je, kutoka mwaka jana 2018 hadi leo, Wizara inasemaje kuhusu kuipandisha Galanos High School?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jambo ambalo Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu (3) Benjamini Mkapa atakumbukwa ni uanzishaji wa Capitation Grants, wa Tsh 12,000 – 10000 kwa kila mwanafunzi kwa mwezi. Kwa sasa kila muda unavyokwenda Capitation Grants inapungua. Naiomba Serikali ilieleze Bunge tatizo ni nini?

Kwa masikitiko makubwa Tanzania imepata taswira mbaya katika medani za elimu katika Afrika na Duniani kwa ujumla kufuatia matukio yafuatayo:-

(a) Mwalimu Mkoani Kagera kumpiga hadi kumuua mwanafunzi wa darasa la tatu bila hatia;

(b) Mwanafunzi wa kidato cha kwanza wiki mbili baada ya mauaji ya mwanafunzi STD III alipigwa hadi kupoteza fahamu;

(c) Mwalimu Mkoani Mbeya amemfunga mwanafunzi miguu juu kichwa chini, amempiga hadi amemvunja mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa matokeo hayo hapo juu ni kielelezo kuwa tunao Walimu ambao hawana sifa ya ualimu bali walitakiwa wawe Field Force Unit (FFU). Naiomba Serikali iliambie Bunge, ina mkakati gani wa kusafisha sekta ya ualimu kwa kuwaondoa Walimu makatili? Zamani wanafunzi wakati tukisoma tulipenda tutakapomaliza shule tutakuwa kama Walimu wetu waliokuwa wakitufundisha, lakini siku hizi imekuwa kinyume, wanafunzi hawapendi kuwa Walimu kwa sababu, Walimu siku hizi wamekuwa wajasiriamali, mwalimu anaenda kazini (shule) amebeba deli la ice cream, chupa ya ladu, kashata, chipsi za mihogo, ubuyu na binjra. Yote hiyo Mwalimu anataka kuongeza kipato kwa kuwa mishahara midogo, wanasomesha watoto, wanahitaji kodi ya nyumba, bili ya maji na umeme. Hivyo naitaka Serikali iongeze mishahara ya Walimu na itamke ni lini itaanza kuongeza mishahara na lini itamaliza kulipa madeni ya Walimu?