Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Rev. Dr. Getrude Pangalile Rwakatare

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane na wenzangu kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri na kwa kazi nzuri sana wanayofanya na timu yake. Kukarabati shule kongwe ni kazi nzuri sana, ajira kwa Walimu wapya, ujenzi wa mabweni kwa watoto wa kike na kutoa elimu bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri kuhusu adhabu ya watoto watoro zaidi ya siku 90 itolewe, pia kwa candidate classes. Hivyo ilivyo inaharibu jina la shule, nafasi ya shule, maana watoto kama hawa hujitokeza siku za mitihani tu. Kukariri darasa kungezingatiwa ili elimu iimarishwe na ukaguzi wa shule uwe wa mara kwa mara.