Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuweza kuchangia hotuba ya elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali mwaka jana bajeti ya Wizara ilikua bilioni 1.408 mwaka huu imeshuka mpaka kufikia bilioni 1.357. Upungufu wa bilioni tano, ni kwa nini Serikali inapunguza bajeti ukiangalia maisha yanapanda, shule zinaongezeka na wanafunzi wanaongezeka na mahitaji yanaongezeka zaidi

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi ya Elimu ya Juu pamoja na bajeti kuongezeka kufikia bilioni 424 ambapo bajeti halisi bilioni 4.3 sawa na asilimia 18 ya bajeti ya maendeleo na mikopo ya wanafunzi asilimia 52 ya bajeti. kuna changamoto ya mikopo ya wanafunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vitambulisho vya Taifa; wanafunzi wanakosa mikopo; kwa hivyo Serikali ishirikiane na NIDA ili wanafunzi wanaostahiki wapate mikopo kwa haraka ili wapate kuendelea na masomo mapema. Vile vile viko vyuo baadhi vina madeni kwa hivyo wanafunzi wanachelewa kupata mikopo hiyo. Kwa hivyo nashauri bodi watumie wanafunzi moja kwa moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyuo vya VETA, Serikali imepanga fedha kidogo sana. Vyuo vya VETA vina mchango mkubwa katika kuleta maendeleo ya vijana wetu kwa sababu vijana wengi wanaomaliza kidato cha nne na wale waliofeli darasa la saba wanataka wajiunge na vyuo hivyo ili kupata ujuzi wa ufundi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka Serikali ya uchumi wa viwanda leo tukiwa na vijana wengi waliopitia vyuo vya VETA watapata ajira. Vile vile tunaishauri Serikali ijenge vyuo vya VETA kila wilaya ili vijana wengi wapate kujiunga na vyuo hivyo.

Baada ya kusema hayo, naomba kuwasilisha.