Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto za mifumo ya elimu ya Tanzania limekuwa tatizo sugu ambalo sasa ni bayana kwamba tunahitaji mbinu tofauti, nyenzo tofauti na mikakati tofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado Serikali haijaamua kutafiti kwa kina kujua nini hasa hitaji la Watanzania kuhusu elimu itakayokidhi. Kipaumbele cha kibajeti kwenda Wizara ya Elimu na Taasisi ya Utafiti ya COSTECH kimekuwa dhaifu na kisichokidhi haja kwa miaka mingi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mitaala yetu inabadilishwa kila siku/kila mara na hivyo kuondoa consistency ya mitaala kwa Walimu na wanafunzi. Hata hivyo, kutowashirikisha Walimu katika suala la uandaaji mitaala, inaondoa ownership na vionjo na mahitaji muhimu ya ufundishaji na kujifunza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016, Serikali ilifanya jitihada kubwa kuhakikisha shule zetu zote nchini zinapata madawati ya kutosha. Ni bahati mbaya sana kuwa kuna shule katika Jiji la Dar es Salaam, licha ya kuwa na msongamano wa wanafunzi madarasani, hazina kabisa madawati. Mfano halisi ni Shule ya Msingi Toangoma iliyoko Kigamboni ambayo ina watoto 540 ambao wanakaa chini. Hili ni jambo la aibu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwango vya elimu vinavyotolewa katika hatua mbalimbali za ukuaji kielimu. Watoto wetu katika shule za msingi wanaosoma katika mazingira dhaifu sana ikiwemo ukosefu wa vitabu vya ziada na kiada, ukosefu wa huduma za maji, umeme na madarasa ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wa hisabati na sayansi, bado ni changamoto. Idadi ya shule imeongezeka wakati hakuna maandalizi kidhi ya Walimu wa kutosha. Tunawaza kuwa Tanzania ya viwanda, lakini ikiwa hakuna Walimu wa kuandaa watoto wetu. Maslahi ya Walimu nayo bado ni kilio kikubwa kiasi kwamba Walimu waliopo kazini wamevunjika moyo sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sehemu kubwa, elimu yetu imekuwa ikitolewa kwa nadharia. Elimu muhimu ni elimu kwa vitendo. Tuboreshe maabara, vyuo vya ufundi viongezwe na mazoezi kwa vitendo yawe sehemu kubwa ya mtaala ili mambo yanayofundishwa yaweze kukaa na kudumu katika fikra za wanafunzi wetu kadri wanavyokua na kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuhamisha Walimu wa Sekondari kurudi kuwa Walimu wa shule za msingi, halikuwa jambo la busara na tumewapeleka kama watu waliodharauliwa na kushushwa thamani na hivyo kutokuwa na moyo wa kufundisha. Kwa hiyo tujue hatujatatua tatizo, tumeliongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.