Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, usahili wa vyuo; Serikali tumeona imefungia baadhi ya vyuo visivyo na sifa hali iliyosababisha usumbufu kwa watoto, wazazi wamepoteza fedha na wanafunzi wamepoteza muda, pia Serikali imechukua hatua gani kulipa fidia kwa usumbufu huo kwa maana hiyo hadi chuo kianze kudahili wanafunzi kuna uzembe pia kwenye mamlaka zilizotoa kibali, je, hatua zipi zimechukuliwa kwa watendaji walioruhusu vyuo hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mlundikano wa wahitimu mtaani ambao hawana ajira, je, Serikali haioni sasa kuna haja kuweka somo la kujitengemea katika vyuo vikuu ili kuwajengea wanafunzi wanaomaliza vyuo kujiajiri wenyewe badala ya kusubiri ajira toka Serikalini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, malalamiko ya Walimu kutopandishwa mishahara na kupanda madaraja bila kupewa haki za kuongeza mishahara yamekuwa ya muda mrefu. Mazingira magumu ya Walimu kuanzia shule za msingi vijijini yanakatisha tama; Serikali kwa nini isije na mpango wa kujenga nyumba za Walimu kama ilivyowahi kuja na mpango kujenga vyumba vya maabara?

Mheshimiwa Mwenyekiti, motivation kwa Walimu wanaojitolea tumeona katika vyombo vya habari, shule za kata zimetoa watoto bora, pia shule za kata Walimu ni wachache wanaofanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhamisho wa Walimu pasipo kulipwa haki na stahili zao; Serikali iliangalie hili, Rais amewahi waambia Walimu wasikubali kuhama kama TAMISEMI haina fedha ya uhamisho. Yapo malalamiko bado ya uhamisho wa Walimu especially Walimu wa sekondari waliopewa shule za msingi kufundisha, Serikalini iangalie upya malalamko hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wengi wapo mijini zaidi kuliko vijijini Serikali iangalie uwezekano wa kuwa na uwiano sawa wa Walimu; inashangaza unakuta shule za msingi vijijini walimu ni wachache, wanalazimika kufanya kazi ngumu kugawana masomo na wengine kulazimika kufundisha masomo wasio na uwezo nayo, hawajasomea mfano sayansi kwa walimu wa Arts. Masomo ya sayansi ndio wanapewa kipaumbele kulinganisha na wanafunzi wanaosoma michepuo mingine.