Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, sera ya elimu haiendani na uhalisia wa elimu yetu ya Tanzania kwa ilivyo sasa. Kwa hiyo naishauri Serikali ilichukue umuhimu wa mabadiliko ya sera ya elimu tuliyonayo hivi sasa ili tuboreshe elimu yetu ya Tanzania kama ilivyokusudiwa mfano, mitaala yetu inaelekeza wanafunzi kukaririshwa na siyo kuelewa na baada ya kuhitimu anafikiria kuajiriwa na si kuendelea na masomo ya juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maslahi ya Walimu yaboreshwe; kama tunahitaji kuboresha elimu yetu ya Tanzania ni lazima maslahi ya Walimu yaboreshwe kwa kuwa ndio wadau wakuu na muhimu wa elimu kwani suala hili ni muhimu sana kwa kuwaletea morari Walimu wetu na pia Walimu hawa wataachana na mawazo ya tuition au kuuza karanga kwa ufupi kuwaza kufanya biashara ndogo ndogo ili kujiongezea kipato cha familia na kusabisha kutofundisha wanafunzi vizuri. Kwa hiyo, naishauri Serikali izingatie jambo hili la kuhusu maslahi ya Walimu kuboreshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Mikopo ibadilishe utaratibu wa michepuko bila kuangalia aina za masomo aliyofaulu bali waangalie alama ambazo mtu (mwanafunzi) amefaulu bila kubagua aina za masomo, kwa mfano, kwa sasa kipaumbele cha Bodi ni kwa wale wanaosoma masomo ya sayansi, ndio wanapewa kipaumbele kulingalisha na wanafunzi wanaosoma michepuo mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuboresha elimu ya Tanzania bila kuboresha kitengo hiki cha Ofisi ya Ukaguzi kukitengea fedha za kutosha kama vile usafiri ili waweze kuyafikia maeneo yote yanayotakiwa kukaguliwa kwa mujibu wa sheria kwa haraka na hii itarahisisha kufikia maeneo yasiyoweza kufikiwa kwa urahisi wakipata usafiri wa uhakika.