Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu kwa kuwa Mtanzania, mwakilishi wa wanawake wa Kilimanjaro Bungeni. Nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu yote ya viongozi wa Idara, Vyuo na Shule zote Nchini kwa juhudi za kutoa elimu bora. Nawapongeza wazazi wote wenye wanafunzi mashuleni na kwenye vyuo ndani na nje ya nchi, pia nawapongeza wanafunzi hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwezesha elimu bila malipo na kuendelea kuteua maprofesa kwenye nafasi mbalimbali jambo hili limewafanya vijana wengi sasa waheshimu elimu na ufaulu mzuri, vilaza sasa wameshastuka kuisha elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ni ufunguo wa maisha, wananchi wakiwa na elimu nzuri, Tanzania ya viwanda itawezekana, maradhi ya kuambukiza yatakwisha, rushwa itapungua au kwisha kabisa, ujambazi utakwisha na mengineyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yangu, Serikali imejiandaa vipi kuwapatia mtaji vijana wanaofuzu vyuo ambao hawajapata ajira ili waanze shughuli za ujasiriamali? Serikali ina mpango gani wa kuwapatia ardhi au maeneo ili vijana kununua viwanja vilivyopimwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya watu wazima, naomba kuisikia Serikali ina mpango gani kuhusu kuendeleza elimu ya watu wazima, yakiwepo mafunzo ya IT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.