Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na niweze kusema. Nianze na suala zima la Bodi ya Mikopo ya wanafunzi, kuna tatizo ambalo linatakiwa lifanyiwe kazi. Tunawakopesha wanafunzi kwa riba kubwa hali ya kwamba wanasomea elimu ambayo hawana uhakika wa kuja kupata ajira na kwa sababu hiyo, itawachukua miaka baada ya kuwa wamehitimu kuja kupata ajira, matokeo yake watakapokuwa wameanza kupata ajira ile riba inakuwa imeongezeka mara dufu kwa hiyo, wanaanza kazi hali ya kwamba wanamzigo mkubwa wa riba ya Bodi ya Mikopo.. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina hakika kama Bodi ya Mikopo inakusudia, inakusudio la kufanya biashara kusudio la Bodi ya Mikopo siyo kufanya biashara, ni kutoa huduma. Kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri tutoe mikopo lakini tupunguze riba, riba ni kubwa sana kubwa mno na kwa sasa mnakata asilimia 15 ya mshahara kwa hiyo mtumishi anaanza kazi lakini kiasi kikubwa cha pesa tayari kinakwenda kwa Bodi ya Mikopo. Kwa hiyo, naomba hili lifanyiwe kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jingine nizungumzie suala zima la wastaafu na stahiki zao. Tunawapandisha watumishi madaraja kwa maandishi tu na siyo vitendo, tunapandisha madaraja hakuna mabadiliko ya mishahara matokeo yake wanapokwenda kwenye kustaafu mafao yao yanakuwa kiduchu. Ni miaka mingi sasa zoezi la upandishaji wa madaraja limekuwa lakubabaisha babaisha watumishi hawa wanaenda kustaafu kwa mafao kidogo kwa sababu wanapandishwa madaraja lakini bila utekelezaji na matokeo ya mafao yao yanakuwa madogo. Kwa hiyo, niombe Wizara ijitahidi kwamba watumishi na hasa wale wanaokaribia kustaafu wapandishwe madaraja ili basi mafao yao yaweze kuwa angalau manono. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine ni suala la elimu bure, hii elimu bure Serikali ijipambanue na iwe wazi elimu bure iwe ni kwa suala zima la ada tu, Serikali iwe wazi iwe wazi kwa wadau wa elimu kuchangia elimu na hasa wazazi tamko la elimu bure limeenda kuharibu uelewa na kiasi kwamba wazazi sasa na hasa wa vijijini huko wanaona kuchangia elimu siyo sawa sawa kwa sababu Sera ya Serikali ni elimu bure. Serikali sasa iwe wazi, iwe wazi kwamba suala la kuchangia elimu ni lazima isipokuwa Serikali yenyewe ubure huu unaozungumzia upo kwenye suala zima la ada tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine nizungumzie suala la elimu ya watu wazima, hasa suala zima la kisomo cha watu wazima. Wakati wa enzi za Baba wa Taifa suala hili lilisisitizwa sana na Tanzania ikawa ni nchi inayopigiwa mfano kwa kuwa imepiga hatua kwenye kuhakikisha kwamba watu wazima wanapata elimu hasa zile skills tatu za kuandika, kuhesabu na kusoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hili jukumu lilipewa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima sasa hivi hii Taasisi inaonekana hili jukumu lake la msingi kana kwamba wameliacha na wamejikita zaidi kwenye hizi elimu rasmi. Katika maeneo yetu bado kuna watu wengi ambao hawajui kusoma hawajui kuhesabu, hawajui kuandika. Na ukisoma kwenye ukurasa ule wa 38 wa Hotuba yako, unasema ndiyo kwanza mmeandaa mkakati wa kuona namna gani mnajikita katika hili eneo. Nasema mmechelewa mfanye haraka bado tuna watu wengi ambao wanahilo tatizo, huo mkakati wenu uwe wa haraka ili basi kuweza kunusuru watu wengi ambao wanamatatizo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine ambalo ningependa niliseme ni suala zima la elimu jumuifu inclusive education. Ukurasa wa 17 umeeleza kwamba Serikali ina mpango mkakati wa kuanzia mwaka 2018/2021 wa kuhakikisha ina mkakati wa hii inclusive education yaani elimu jumuishi lakini mpaka sasa hivi mko katika hatua ya uchapishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona hili suala kama limechelewa sana na tunaposema inclusive education ni nini. Huu ni mpango ambao wanafunzi wa aina yote wale walio na ulemavu na wasio na ulemavu watafundishwa katika darasa moja. Kimsingi suala hili kama litafuatiliwa na kutekeleza litawasaidia sana na litawasaidia sana walemavu kwa sababu kwa kufanya hivyo walemavu wanaweza waka- coop na kujifunza kutoka kwa wenzao ambao wasio walemavu. Lakini kwa kufanya hivyo na wale ambao wasio na ulemavu watakuwa familia na wale wenye ulemavu. Huu ni mpango mzuri sana lakini mpaka sasa inaonekana limezungumziwa kwa miaka mingi lakini utekelezaji wake unachelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe na niishauri Wizara suala hili ni zuri na lifanyike kwa haraka lakini liendane sambamba pamoja na kutoa mafunzo kwa wale walimu ambao hawa-skills za kuwafundisha walemavu. Liendane sambamba na kutoa motisha kwa walimu ambao wataenda kuwafundisha watoto walemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini liendane sambamba na kuwa na idadi kubwa ya walimu katika darasa hilo, kwa sababu katika darasa ambalo linawatoto walemavu na wasiowalemavu, kuwa na mwalimu mmoja ni mtihani lazima kuwepo na mwalimu ambaye hana hiyo skills za kuwafundisha watoto walemavu na yule ambaye ni mwalimu wa elimu maalum. Suala hilo naomba Serikali ilifanye kwa haraka kwasababu kundi hili la watu wenye ulemavu linaendelea kutengwa na kunakuwa na tendency ya kuwa na over protection lakini kunakuwa na tendency ya isolation kwa hiyo tukiwachanganya hawa itawasaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna suala zima la maslahi ya walimu. Walimu hawa wamekuwa wakifanya kazi kubwa kwa ari lakini bado Serikali haijaona namna gari inaweza kuwamotisha. Niombe Serikali itakapokuja basi itoe matumaini kwa walimu kwa kuongeza mishahara yao lakini itoe motisha kwa walimu kwa kuongeza madaraja yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala zima la teaching allowance, teaching allowance Mheshimiwa Ndalichako wewe ni mwalimu kazi ya ualimu ni kazi nzito, walimu tulivushe hili kundi basi lazima tuone uwezekano wa kuwapa teaching allowance kitu hiki kitawasaidia sana na kilifanyika wakati wa mzee Mwinyi teaching allowance inawezekana katika kipindi hiki cha Mheshimiwa Dkt. Magufuli, na hilo mtaliweza kama mnaweza kufanya mambo makubwa makubwa na mazito mazito, fanyeni hili kwa walimu basi, fanyeni tuwarushie hiyo teaching allowance. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala zima la Sera ya Elimu. Wakati wa Baba wa Taifa, Sera yetu ya elimu ilikuwa education for self-reliance elimu inayotolewa basi imuandae mwanafunzi aweze kujitegemea lakini sasa sera yetu na muundo wetu wa elimu ni kama haueleweki, tunatoa elimu tuna watu wanahitimu lakini hawana uwezo wa kujitegemea sasa hivi tumekuwa na fashion ya kuwa na vyuo vingi vinavyotoa degree lakini baada ya kuwa tumekamilisha wanafunzi hawa wamepata degree hawawezi kujitegemea. Kwa hiyo, lazima tuje na mitaala ambayo itamuandaa mwanafunzi ili aweze kujitegemea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana ahsante sana. (Makofi)