Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kutoa mawazo yangu kwa Wizara muhimu sana, Wizara ya Elimu. Awali ya yote, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Mheshimiwa Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa mchango mkubwa ambao mnautoa kwenye Wizara yenu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Taifa tumekuwa na matamanio sasa ya muda kuhakikisha nchi yetu inafikia uchumi wa kati. Ni imani yangu na ya Watanzania wengi kuwa Wizara ya Elimu ni kiungo kikubwa ambacho kitatusaidia sisi kuweza kufikia malengo hayo ya uchumi wa kati na ambayo yataendeshwa kwa viwanda na biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema haya? Wizara ya Elimu ndiyo iliyopewa jukumu la kuandaa Sera ya Elimu nchini, mitaala ambayo ita-reflect pale ambapo sisi Watanzania tunataka kufikia na kuandaa walimu ambao tunategemea watakuwa na hizi skills na knowledge ambapo wata-transfer kwa hawa watoto wetu ambao tunategemea waje waweze kuendesha hivi viwanda ambavyo tayari vimeanzishwa kwenye mikoa yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha hoja yake kesho angetueleza Wizara ya Elimu, Sera ya Elimu hapa nchini ni nini? Je, sera na mitaala ambayo tumeiandaa inaweza kuwasaidia hawa vijana kutimiza malengo yao? Let’s say watoto ambao wata- graduate miaka mitano ijayo anaweza akatumia hizi skills na utaalam ambao amepata shuleni kufanya kazi kwenye viwanda hivi? Je, huu ujuzi alioupata anaweza akatumia fursa zilizopo akaanzisha biashara, akajikita kwenye kilimo chenye tija, akawa mfugaji badala ya sasa ambao asilimia kubwa ya vijana wanategemea kuajiriwa Serikalini? Hilo ni jambo la msingi sana Mheshimiwa Waziri, napenda ulitolee maelekezo ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ya pili, nilitaka tujue sasa kama Wizara tumejiandaa vipi kuhakikisha hawa walimu ambao nimesema ndiyo nguzo muhimu wameandaliwa kuhakikisha wana utaalam wa kutosha kuweza kuwafikisha hawa watoto hapo ambapo tunataka wafikie. I stand to be corrected, nakumbuka kwenye hotuba ya bejeti ya mwaka 2018/2019 ilionesha kabisa tuna upungufu wa walimu hasa shule za msingi, nakumbuka idadi ilikuwa zaidi ya 85,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali kuwa mwaka huu tumeweza kuajiri hao walimu 4,500 lakini ni wachache, hawawezi kukidhi shida ambayo tunayo sasa hivi na walimu wapo. Nakumbuka Waziri wa TAMISEMI alivyotangaza ajira hizi, zaidi ya walimu 90,000 walituma application kupata nafasi hizi za kazi.

Kwa hiyo, tushirikiane na Wizara ya TAMISEMI tuhakikishe tunaajiri walimu wa kutosha. Hali ya walimu kwenye maeneo yetu hasa Mkoa wa Iringa bado ni changamoto kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili walimu wetu wawe na ufanisi wa kufundisha lazima workload yao iwe ndogo, uwiano kati ya walimu na wanafunzi lazima uwe mzuri. Nitatoa mfano, kwa walimu wa shule ya awali inakadiriwa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 189, in average tunatakiwa tuwe na mwalimu mmoja kwa watoto 25. Kwa hiyo, tumeanza kuajiri ni jambo jema lakini tusiishie hapo, tuna jukumu la kuhakikisha tunaajiri walimu wa kutosha ili wawe na uwezo wa kufundisha hawa watoto wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii workload waliyokuwa nayo tumeona inavunja morale. Hata hawa ambao sasa hivi wanakwenda kufundisha, wakifika kule kwa workload iliyopo ni vigumu wao kufanya followup, kuhakikisha hawa watoto wame-grasp hizi concept ambazo wanawafundisha darasani. Kwa hiyo, tunajikuta tuna walimu nusu, nadhani watu wa Hakielimu walionesha last year, less than 40% walimu wako motivated kufundisha darasani. Sasa tutapaleka hao walimu wako pale lakini kumbe zaidi ya nusu hawana morale ya kufundisha watoto wetu. Kwa hiyo, tunatakiwa tufanye jitihada za makusudi kuhakikisha jambo hili tunaliweka vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Serikali utakuwa kama ufuatavyo. Kama nilivyosema walimu ni kiungo kikubwa sana sasa tuhakikishe in-service training tukishirikiana na Wizara ya TAMISEMI tunawaendeleza hawa walimu wetu. Kama Wizara mmekuwa mnatoa miongozo mbalimbali, tunabadilisha mitaala, je, hawa walimu wako trained kuhakikisha wanaenda na hiyo miongozo na mitaala mipya ambayo mmeileta? Kwa hiyo, tuhakikishe in-service training inakuwepo kwa walimu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile issue ya IT (Information Technology), ni lazima kama nchi tuanze hii conversation, hatuwezi kukwepa. Wenzetu wa Rwanda sasa hivi wameshaanza, Kenya wameshaanza haya majadiliano, najua ni gharama na itakuwa ni kazi kubwa lakini lazima tuanze. Hivi viwanda tunavyoanzisha lazima tuwe na vijana ambao wako multiskilled. Tutaanzisha viwanda tutaishia kuchukua expert’s kutoka nchi za nje kuja kufanya kazi kwenye viwanda vyetu. Inasikitisha mtoto anakuja kuona desktop au tablet anapofika labda chuo, lazima hawa watoto wawe exposed kwenye hizi sayansi na teknolojia mapema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama nilivyosema, issue ni kubwa, we have to start somewhere at least tuwe na conversation. Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa kuhitimisha atueleze tuone inakuwaje. Uzuri sasa hivi tuna umeme mpaka vijijini, kwa hiyo, tuna access ya kuweka hata computer moja moja kwenye shule ili watoto wawe exposed kwenye hizi new technology. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Mheshimiwa Waziri ana uwezo (competent) wa kututoa hapa tulipo kwa kutengeneza sera na mitaala yetu mizuri ili tuweze kufika pale ambapo tunataka kufika kwenye uchumi wa kati. Tuhakikishe tunaajiri walimu wa kutosha, tuwawezeshe, tuna uwezo wa kufika huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nimtakie kheri Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara katika utekelezaji wa bajeti hii. Nashukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)