Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Rev. Dr. Getrude Pangalile Rwakatare

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MCH. DKT. GERTRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote niipongeze Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya. Nimpongeze sana Waziri Mheshimiwa Kangi Lugola kwa kazi nzuri wanayoifanya. Ujambazi umepungua kwa kiasi kikubwa sana, tunatembea kwa uhuru, ajali za barabarani zimepungua mno na uvamizi wa mabenki pia umepungua sana. Hongereni.

Mheshimiwa Spika, naomba nyumba za askari Ifakara - Kilombero zijengwe, wana shida kubwa ya makazi. Pia tunaomba Mahakama ya Ifakara ijengwe, wakati wa masika, mafuriko yanaathiri wafungwa, mafaili, ofisi na ni kero kubwa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja mia kwa mia.