Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Spika, vitendea kazi vya Polisi. Jimbo la Simanjiro lina ukubwa wa square kilometer 21,000 takriban gari moja kwa wilaya kubwa kama hii, ni mateso na ni ngumu sana. Naomba jimbo hili liangaliwe kwa karibu. Kwa ukubwa huo Wilaya ya Simanjiro ni vyema pia mafuta ya mwezi wakaongezewa kutokana na ukubwa wa eneo husika.

Mheshimiwa Spika, kesi zisizo na tija; Polisi Kituo cha Msitu na Tembo eneo ambalo lina rasilimali ya asili (Mto wa Nyumba ya Mungu) Mkuu wa kituo kile amekuwa na tabia ya kubambikiza wananchi kesi kwa sababu zisizo za msingi.

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe mfano mmoja wa mtu mmoja tajiri anayedhulumu wananchi wa Loliondo ardhi yao lakini Mkuu wa Kituo hiki ili kutuliza madai ya wananchi kutetea ardhi yao, ameamua kimkakati kushirikiana na tajiri huyo anayedhulumu wananchi eneo lao, kuwafungulia kesi nyingi sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kupongeza Jeshi la Polisi kwa ujumla wake kwa kazi nzuri inayofanywa na kikosi chini ya IGP Sirro. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri. Tunayo amani ya kutosha na eneo la Mererani ambalo hapo awali lilikuwa na matukio mabaya, kwa sasa lina amani ya kutosha. Ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, maaskari wasio waadilifu; ni vyema Wizara hii ilinde taswira ya Jeshi la Polisi kwa kuwaadhibu maaskari ambao sio waaminifu ili kulinda heshima ya Jeshi la Polisi. Polisi ni taswira ya nchi yetu. Naomba wahudumiwe kwa uhakika na mahitaji yao yaangaliwe na Wizara.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii ya muhimu. Nawatakia kheri kwenye utekelezaji wa majukumu yao.