Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, kumekuwepo na kauli mpya tata na zenye ukakasi zinazotolewa na Jeshi la Polisi kwa siku za hivi karibuni; mfano, tutawapiga mpaka mchakae – RPC Muroto; tutapiga vipigo vya mbwa koko na nyingine zenye ukakasi kama hizo. Tafsiri ya kauli hizi ni ulevi wa madaraka, ubaguzi na kuwa juu ya sheria.

Mheshimiwa Spika, kauli hizi hazisikiki tu kwa Jeshi la Polisi na hata kwa wanasiasa kama Mkuu wa Mkoa wa Tabora, akimtaka Mungu amshukuru Rais Magufuli na mengine kama haya. Ulevi wa madaraka, lakini kauli hizi zitafsiriwe kama zinaungwa mkono na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuwa, haiamini tena katika Government of the People for the People by the People.

Mheshimiwa Spika, Fungu Namba 28 – Polisi, limekuwa na upungufu mwingi sana katika matumizi ya fedha na haya yamesemwa na CAG Report 2012/2013 mpaka leo hii. Mfano, zoezi la ujenzi wa vituo vya Polisi vya mfano chini ya mradi wa STACA uliodhaminiwa na Serikali ya Uingereza ukiwa na thamani ya zaidi ya pound milioni tatu (Tsh. 10 billion). Ujenzi wa hivyo vituo ulienda kinyume na MOU.

(1) Budget ya estimates haikuendana na actual implementation. Bajeti ya kukarabati vituo 35 vilikarabatiwa 16 tu ambayo ni asilimia 46 ya kazi.

(2) Ripoti za uwongo, mfano taarifa ya 2012/2013 kukamilika vituo vya Nachingwea, Nyakato na Kondoa.

(3) Ripoti ya 2013/2014 ilionesha hakuna kazi iliyofanyika katika vituo hivyo na walienda site hawakuona chochote.

(4) Mwaka 2014/2015 hakukuwa na ripoti iliyotolewa.

(5) Ujenzi wa vituo vingine bila mikataba na wakandarasi, mfano, M/S Posh-alliance kiasi cha Sh. 515,233,760.

(6) Ufisadi katika ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Mfano Makambako (Model Police Station).

(7) Milioni 25 zililipwa kwa mkandarasi kwa ununuzi wa fenicha ambazo hazikununuliwa.

(8) kupotea kwa fedha ya wananchi mikononi mwa Polisi, wanaowekwa mahabusu au zinazokuwa vidhibiti; Tsh. 145,410; Ksh. 25,900 na Euro 800.

(9) Delay in banking revenue collected of Tsh. 93,725,000. Delay in submission of revenue collected na traffic notification of over 24 million.

(10) Kushindwa kukusanya fines zenye thamani ya zaidi ya bilioni 4.4.

(11) Walifanya malipo ya milioni 234, zaidi kwa watoa huduma waliokuwa hawastahili, Time General Supplies.

(12) Malipo kwa watoa huduma ya milioni 103.4 bila kushindanishwa. Single source procurement million 179.4; total of zaidi ya milioni 700 zimekiuka taratibu za manunuzi.

(13) Matumizi ya zaidi ya milioni 345.9 ambazo hazikuidhinishwa na IGP kuanzia 2013 – 2017 na bila vithibitisho kinyume na PGO 121(2).

(14) Matumizi yasiyoeleweka ya kikao cha Viongozi Wakuu kilichofanyika Dodoma tarehe 17 – 19 Aprili, 2017 zaidi ya milioni 156,206,000 zilitumika na hazikuwa na ushahidi out of 246.03 verification ilifanyika kwa milioni 89.8 tu.