Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, kwanza naanza kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoifanya kwa Ulinzi na Usalama wa nchi hii.

Mheshimiwa Spika, pia nampongeza Mheshimiwa Kangi Lugola, Waziri na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Masauni, sisi Jimbo la Mbulu Vijijini tumejenga Kituo cha Polisi cha Yaeda Chini na kukimaliza kabisa tumebakia na nyumba za Walimu ili kituo kianzishwe hapo Yaeda Chini kwani wananchi wamejenga ili kupata usalama wa watu na mali zao. Sababu za kujenga kituo pametokea mauaji ya raia hapo nyuma bila watuhumiwa kufikishwa Mahakamani.

Mheshimiwa Spika, kuna wizi wa mifugo ambao unaendelea, mifugo mingi imekuwa ikiibiwa na ikawaacha wananchi wakiwa hawana nchi zao ndiyo maana wameamua kujenga kituo cha polisi. Wanawake wengi wamekuwa wanabakwa sana hii ni kutokana na taarifa ambazo zipo. Ili kupunguza tatizo hilo tume ambazo zipo ili kupunguza tatizo hilo tumeamka kujenga kituo cha polisi ila tumeishiwa na nguvu za kuweza kuchangia hela na nyumba za askari tusaidieni hata nyumba moja. Mimi Mbunge nimechanga milioni nane za ujenzi wa kituo hiki cha polisi kushirikiana na wananchi. Ombi langu tupatiwe fedha za ujenzi wa nyumba za askari.