Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Kangi Lugola pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri Engineer Yussuf Masauni kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi nzuri wanayoifanya, naomba nipewe majibu sababu zipi zinasababisha askari wote wenye cheo cha nyota moja kushuka chini wamewekewa ukomo wa kustaafu miaka 55. Hii sheria au kanuni haiwatendei haki askari hao; kwa nini Serikali isiangalie upya utaratibu huu na kuwaweka katika utaratibu wa miaka 60 kama ulivyo kwenye maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.