Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Makame Mashaka Foum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MAKAME MASHAKA FOUM: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mungu kunijaalia afya njema, namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri ya kutekeleza majukumu ya kulijenga Taifa letu. Pia namshukuru Waziri na Watendaji wote wa Wizara hii, amani na utulivu tulionao ni kutokana na Jeshi letu.

Mheshimiwa Spika, watu wengi wanafanya makosa kutokana na kutozijua sharia, hivyo naiomba Wizara itumie njia mbalimbali za kuelimisha jamii ili iepukane na kutenda makosa.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Jeshi la Magereza, naishauri Wizara kupanga mikakati na mipango mizuri ya kuhakikisha Jeshi la Magereza linazalisha chakula cha kutosha kujitosheleza. Sambamba na hilo wanayo maeneo mazuri kwa ajili ya mifugo. Naamini tunaweza kutoa maziwa, nyama na kadhalika kutokana na mifugo.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali pesa za maendeleo zipelekwe kwa wakati ili kutatua changamoto za majengo. Askari wetu wengi wanaishi katika nyumba duni, ili waweze kufanya kazi vizuri tuhakikishe wanapatiwa mazingira mazuri ya kuishi, Askari wetu wengi wanaishi katika mazingira magumu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.