Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, niongelee kuhusu vifo vinavyotokana na ukatili wa Jeshi la Polisi. Hivi karibuni kumekuwa na matukio ya wananchi kunyanyaswa na baadhi ya Polisi na kuripotiwa katika maeneo mbalimbali. Mfano, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Vijijni (Tanganyika) amekuwa akitumia baadhi ya Askari kunyanyasa wananchi wa Tanganyika. Wananchi wanawekwa ndani (rumande) wanabambikiziwa kesi mbalimbali, wanachomewa nyumba kwa maelekezo ya Mhando.

Mheshimiwa Spika, mmoja kati ya wananchi waliopigwa risasi na Askari na kufa anaitwa Shinje, Aprili, mwaka 2018. Jambo hili na mengineyo yanayoendelea kutokea katika mkoa wetu, yanachafua Jeshi la Polisi, lakini pia Serikali kupitia Jeshi la Polisi inashindwa kulinda mali za raia wake na usalama wao. Hii inapelekea watu kutokuwa na imani na jeshi la polisi.

Mheshimiwa Spika, nataka Mheshimiwa Waziri akija hapa, ajibu ni kwa nini baadhi ya Askari wanafanya uovu na hawachukuliwi hatua; Wakuu wa Wilaya hawa Mheshimiwa Mhando wa Tanganyika na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda? Je, sheria za kutoa amri kwa Polisi kuwakamata raia wanatoa wapi wateuliwa hawa? Jambo hili linakera na lisipofanyiwa kazi linaenda kuleta athari kubwa.

Mheshimiwa Spika, kingine ni kuhusu upotevu wa mali za raia katika vituo, vifaa vya raia vinavyokamatwa na Polisi, pikipiki, TV, Redio vitu vingine. Hii imekuwa ni kero kwa sababu unakuta mtuhumiwa anakamatwa; ushahidi na kesi inaenda Mahakamani, lakini baada ya muda vitu vya ushahidi vinapotea, vinauzwa au unakuta mali za wananchi ziko mtaani. Mheshimiwa Waziri ajibu, hili linakera na kuchafua Jeshi hili ambalo linatumika vibaya na baadhi ya Polisi wasio waaminifu.

Mheshimiwa Spika, ni kwa nini RCO, Wakuu wa Vituo wanazuia Mikutano ya Hadhara na huku Polepole anaachwa akifanya mikutano ya ndani na nje? Intelijensia inapatikana kwa viongozi wa Upinzani tu ila kwa CCM hawapatikani na taarifa za intelijensia ambazo ni mbaya.