Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Spika, zoezi la Vitambulisho vya Taifa kwenye Jimbo la Mikumi, zoezi la uandikishaji wa hivi vitambulisho vya Taifa limesimama kabisa. Jimboni Mikumi na Wilaya ya Kilosa kwa ujumla watu walishalipa fedha zao, shilingi 500/= kila mmoja lakini mpaka leo bado hawajapewa Vitambulisho vyao vya Taifa na mbaya zaidi hili tamko la Serikali kuhusu kusajili namba zote za simu nchini ukiwa na kitambulisho cha Taifa imeleta sintofahamu kubwa sana kwa wananchi wetu na Watanzania kwa ujumla. Naomba Waziri wa Mambo ya Ndani akija kuhitimisha atoe kauli ya Serikali kuhusu zoezi hili la vitambulisho na usajili wa namba za simu kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, upotevu wa wananchi kumi wa Kijiji cha Ruhembe Jimbo la Mikumi; niliripoti Bungeni na kwenye vyombo mbalimbali vya usalama na vyombo vya habari kuhusu watu 10 waliopotea wakiwa pembezoni wa Hifadhi ya Mikumi, lakini mpaka leo tarehe 24 bado hakuna majibu ya Serikali kama hawa watu ni wazima, wamekamatwa au wamekufa tangu walipopotea tarehe 2 Aprili, 2019. Je, Waziri wa Mambo ya Ndani na vyombo vyake vya ulinzi na usalama wanatoa kauli gani juu ya upotevu wa ndugu zetu hawa?

Mheshimiwa Spika, baada ya kuwa na migogoro mfululizo ya wakulima na wafugaji Wilayani Kilosa, Serikali iliahidi kujenga vituo vya Polisi kwenye Kata za Tindiga, Ulaya, Kilangali, Malolo na Mabwerebwere: Je, Serikali itatimiza lini ahadi yake hiyo ya kulinda wananchi na mali zao kwenye kata hizi?

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi Mikumi ni muhimu sana na kina kazi kubwa sana ya kulinda wananchi wa Tarafa nzima ya Mikumi yenye Kata saba za Mikumi, Malalo, Uleling’ombe, Mhenda, Ulaya, Kisanga na ukizingatia Mikumi ni Mji Mdogo wa Kitalii na idadi kubwa sana ya watu, kituo hiki hakina gari ya doria na mbaya zaidi Cell yao ni ndogo sana. Hakuna choo na mpaka leo watuhumiwa wanajisaidia kwenye ndoo. Naomba sana Mheshimiwa Waziri akitupie jicho la huruma kituo hiki cha Mikumi ili Askari wetu waweze kufanya kazi yao kwa weledi na watuhumiwa wapate haki yao ya mazingira salama.