Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Spika, mazingira ya kufanyika mikutano ya hadhara kwa Vyama vya Upinzani inaonekana kukataliwa na kutoruhusiwa mara nyingi na Jeshi la Polisi. Hivyo, kitendo hiki kinanyima fursa ya kidemokrasia kwa kukandamiza uhuru wa Vyama vya Upinzani. Je, Polisi sasa wana mkakati gani wa kuondokana na dosari hii?

Mheshimiwa Spika, msongamano wa mahabusu na wafungwa kwenye Magereza bado ni mkubwa na hii inatokana na upelelezi kuchukua muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, kesi ya Mashehe wa Uamsho imechukua muda wa miaka sita sasa bila kujua hatma yao ni ipi, kwani hadi leo upelelezi haujakamilika. Ninaomba jambo hili vyombo vinavyohusika hasa wanaotafuta upelelezi lifanywe haraka ili haki itendeke.

Mheshimiwa Spika, mchakato wa kupatikana kwa vitambulisho vya Mtanzania bado haujaridhisha, kwani unaonekana ni ndoto kwamba hadi kufikia 2020 kupatikana kwa vitambulisho hivyo kwa Watanzania wote. Ninashauri Serikali iongeze mtambo wa kuzalisha Vitambulisho vya Taifa.

Mheshimiwa Spika, ubovu wa Kituo cha Konde, Pemba unatisha. Mvua zikinyesha maji yanahatarisha afya ya Askari. Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati kituo hicho na Kituo cha Matongatuoni, Pemba ambacho ni kibovu?

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.